Tanzania yapata heshima WSIS 2026 ubunifu kidijitali

USWIS: Tanzania imeendelea kupata mafanikio makubwa katika utekelezaji wa ajenda ya mageuzi ya kidijitali, yakidhihirisha dhamira ya Serikali ya kujenga uchumi wa kidijitali jumuishi unaowanufaisha wananchi.

Kutokana na hatua hizo, Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kupitia Mradi wa JamiiStack imetambuliwa katika Tuzo za WSIS Prizes 2026 zinazofanyika Geneva, Uswisi, katika Kongamano la Kimataifa kuhusu Jamii ya Habari (WSIS 2026) zikitambua miradi na ubunifu unaochangia maendeleo endelevu kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.
Mafanikio hayo yanatokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa nchini Tanzania katika miundombinu ya TEHAMA, uboreshaji wa huduma za umma kwa njia za kidijitali na kuimarika kwa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi na wadau wa maendeleo.



