Myanmar yaongeza muda wa tahadhari

MYANMAR: SERIKALI ya kijeshi ya Myanmar yarefusha hali ya tahadhari kwa miezi sita zaidi, huku ikiwa ni miaka minne tangu iliponyakua madaraka kwa nguvu na kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Baraza hilo lilioongozwa na Mkuu wa Jeshi, Min Aung Hlaing, liliidhinisha uamuzi huu, ambao unazuia uchaguzi ulioahidiwa kufanyika mapema.
Uchaguzi sasa unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa nusu ya pili ya mwaka, baada ya mapinduzi ya Februari 1, 2021, yaliyoondoa chama cha NLD cha Aung San Suu Kyi.



