Katimba-Uchaguzi upite,umoja ubaki

KIGOMA: NAIBU Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Zainab Katimba, amewataka Watanzania kutokubali kupoteza amani yao au kufarakana kutokana na tofauti za kisiasa zinazojitokeza wakati wa uchaguzi.

Amesema kuwa chaguzi ni za muda na hupita, lakini mahusiano ya kidugu na kitaifa ni ya kudumu na ndiyo msingi wa mshikamano wa taifa. Akizungumza akiwa Mgeni Rasmi katika maadhimisho ya Maulid ya kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW) yaliyoandaliwa na Msikiti wa Muumin, Ujiji mkoani Kigoma, Katimba amewahimiza Watanzania kushiriki michakato ya uchaguzi kwa amani bila ugomvi.

Naibu Waziri huyo alisisitiza kuwa serikali imeweka sheria na taratibu za uchaguzi ambazo kila mmoja kuanzia wagombea, viongozi wa vyama hadi wananchi wa kawaida anatakiwa kuzingatia. Amesema uchaguzi wa kistaarabu unahitaji kila mtu kusimama kwenye nafasi yake, kufanya maamuzi kwa busara na kuepuka jazba. SOMA: Amani iendelee kutawala kampeni Uchaguzi Mkuu

Naye Kadhi wa Mkoa Kigoma, AbdulMuhsin Kitumba, alisema Maulid ni siku muhimu kwa Waislamu duniani kote, kwani ni fursa ya kukumbuka na kuenzi maisha mema na mafundisho ya Mtume Muhammad (SAW), ambayo waumini wanapaswa kuyaishi kila siku.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. Google pays $300 on a regular basis. My latest salary check was $8600 for working 10 hours a week on the internet. My younger sibling has been averaging $19k for the last few months, and he constantly works approximately 24 hours. I’m not sure how simple it was once I checked it out.

    This is my main concern……………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. I just worked part-time from my apartment for 5 weeks, but I made $30,030. I lost my former business and was soon worn out. Thank goodness, I found this employment online and I was able to Haa start working from home right away. This top career is achievable by everyone, and it will improve their online revenue by:.
    .
    EXTRA DETAILS HERE:>>> https://work99.site

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button