CUF yatangaza vipaumbele 13 Morogoro

MOROGORO : MGOMBEA ubunge wa Jimbo la Morogoro Mjini kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Nyambi Athuman amesema endapo wananchi watamchangua kuwa mbunge wao atasimamia utekelezaji wa Ilani ya chama chake yenye maeneo 13 ya vipaumbele.

Maeneo hayo ya vipaumbele ni pamoja na uboreshaji wa huduma za afya, elimu, maji na miundombinu ambayo ni maono ya kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), ifikapo mwaka 2030. Mgombea wa ubunge huyo alisema hayo katika mkutano uzunduzi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu uliofanyika eneo la Soko la Mawenzi, Manispaa ya Morogoro juzi.

Alisema CUF inaamini katika falsafa ya ‘Haki Sawa kwa Wote’ inahakikisha kila mwananchi anapata haki zake za kiuchumi, kijamii, mazingira bora na kipato cha msingi. Mgombea huyo alisema katika ilani hiyo imeelekeza kuboresha afya njema hususani kwa akina mama wajawazito na watoto kwa kupatiwa huduma bure, ustawi wa jamii, elimu bora kuanzia awali hadi chuo kikuu na jumuishi, kusimamia usawa wa kijinsia na haki za kundi maalumu.

Alisema endapo atachaguliwa atahakikisha anasimamia ilani hiyo ambayo imeelekeza hatua mbalimbali zikiwemo za kuboresha huduma ya maji safi na usafi wa mazingira. SOMA: Mgombea urais CUF: Pigeni kura, msisuse

Alitaja maeneo ya vipaumbele katika ilani hiyo ni kutokomeza umasikini kwa kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia vikundi vya uzalishaji mali, SACCOS na huduma jumuishi za kifedha. Pia, kupanua ajira nadhifu kupitia programu za kilimo, biashara ndogo za kazi na viwanda vidogo na kuanzisha mpango wa ruzuku ya huduma za msingi kwa familia masikini.

Alivitaja vipaumbele vingine ni kutokomeza njaa, kukuza kilimo endelevu hususani uboreshaji wa huduma za ugani, pembejeo za kisasa kwa wakulima, kuendeleza kilimo cha umwagiliaji maeneo ya mabonde, kuwezesha masoko ya uhakika ya mazao kwa wakulima kupitia ushirika na mifumo ya kidijiti.

Naye Mwenyekiti mstaafu wa CUF Wilaya ya Morogoro kichama, Abeid Mlapakolo akimtambulisha na kumdani mgombea huyo wa ubunge alisema suala la upigaji kura ni haki ya wananchi.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

    1. I’m making over $25,000 a month working part-time. I kept hearing other people talk about how much money they were making online, so I decided to look into it. Well, it’s all true and has completely changed my life. This is what I do. Check it out by visiting the following link:

      COPY THIS →→→→ http://Www.Cashprofit7.Site

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button