Wakazi mijini hatarini uchafuzi wa hewa

UCHAFUZI wa hewa umeendelea kuwa tishio kubwa kwa afya ya wananchi nchini Tanzania.Tafiti za hivi karibuni zinaonesha kuwa viwango vya juu vya uchafuzi vinakumba miji mikubwa kama Dar es Salaam, huku athari zake zikikumba hasa watoto, wajawazito, na watu wanaoishi katika maeneo yenye shughuli nyingi za viwanda na usafiri.

Kwa mujibu wa Ripoti ya Health Effects Institute (HEI) ya mwaka 2025 inaeleza kuwa: “Uchafuzi wa hewa ni sababu kuu ya pili inayosababisha vifo katika ukanda huu wa Afrika Mashariki, ikiwa na vifo takribani 294,000 mwaka 2021.” SOMA: Milioni 400 kukabiliana mabadiliko ya tabianchi

Aidha, tafiti zinaonesha kuwa “watoto katika maeneo ya Dar es Salaam wanakumbwa na dalili za magonjwa ya kupumua kama kikohozi, kupumua kwa shida, na pumu, kutokana na viwango vya juu vya PM2.5 na PM10.”

Ripoti nyingine ya Shirika la Afya Duniani (WH0) inasema: “Vifo 60 kwa kila watu 100,000 vinahusishwa na uchafuzi wa hewa wa ndani kila mwaka nchini Tanzania. ” Hali hii inatishia afya ya jamii na inaashiria umuhimu wa kuchukua hatua za haraka.”

Watafiti na wadau wa afya wanasisitiza kuwa serikali lazima iimarishe sheria za udhibiti wa uchafuzi wa hewa na kuhakikisha utekelezaji wake unafanikishwa. Kwa kufanya hivyo, Tanzania inaweza kupunguza athari za uchafuzi wa hewa https://www.instagram.com/reel/DHG915RqpMi/?hl=enna kulinda afya ya wananchi wake, huku ikiimarisha usalama wa mazingira kwa vizazi vijavyo.

 

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  2. Google pays $220 an hour online. My close relative had been unemployed for nine months, but last month, she received a $25k paycheck by working from home for 10 hours a day. Everyone should try this job now—just use this link. COPY THIS →→→→ https://Www.Salary7.Zone

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button