Sirro ahimiza masomo ya sayansi sekondari

KIGOMA: Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Balozi Simon Sirro amewataka wazazi mkoani Kigoma kuhamasisha watoto wao kuyapenda masomo ya sayansi ili kuzalisha idadi kubwa ya wataalamu.

Balozi Sirro ametoa amesema hayo wakati akikagua ujenzi wa maabara tatu za  masomo ya kemia, baiolojia na fizikia katika Shule ya Sekondari ya  Kakonko mkoani Kigoma ukiwa ni moja ya miradi inayotekelezwa  na Shirika la Umoja  wa Mataifa la kuhudumia watoto (UNICEF)  kupitia Mamlaka ya Elimu Tanzania(TEA) kwa gharama ya Sh milioni 180.

Mkuu huyo wa mkoa amesema kuwa serikali imekuwa ikihimiza wanafunzi kusoma masomo ya sayansi na kutoa ufadhili kwa wanafunzi wanaofanya vizuri ili kusaidia kuongeza morali ya kuinua wanafunzi kusoma masomo ya sayansi na kupata idadi kubwa ya wataalam wanaotokana na kozi mbalimbali zinazotokana na masomo ya sayansi.

Amesema kuwa wazazi wana jukumu kubwa kuwahimiza na kuwaandaa watoto wao kusoma masomo yao sayansi sambamba na kuwasaidia katika kuwawekea mazingira mazuri ambayo watoto watasoma masomo hayo na kuyapenda.

Akizungumzia ujenzi wa maabara hizo Mkuu huyo wa mkoa Kigoma amewataka wanafunzi, wazazi na jumuia nzima ya shule hiyo kuilinda na kuitunza miundombinu hiyo  muhimu ya kujifunzia na kufundishia  ili iweze kutumika kwa muda mrefu na kunufaisha kundi kubwa la watanzania.

Awali Mkuu wa Shule hiyo, Anatoria Paul alisema  kuwa kukamilika kwa mradi huo kumeongeza hamasa kwa wanafunzi wengi kusoma masomo ya Sayansi sambamba na kufanya vizuri katika masomo hayo kutokana na kuwepo kwa vifaa kutosha vya kujifunzia na kufundishia.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button