Upandaji miti ni uhai wa mazingira

WASWAHILI husema, “Mchumia juani, hulia kivulini,” wakimaanisha kuwa mafanikio huletwa na juhudi. Methali hii inaakisi umuhimu wa upandaji miti katika jamii ili kujipatia manufaa ya kivuli, mvua, pamoja na mazingira salama.

Jamii nchini imetakiwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za upandaji miti ili kusaidia utunzaji na uhifadhi wa mazingira ambayo kwa sasa yanakumbwa na changamoto nyingi zikiwemo mmomonyoko wa udongo na mafuriko.

Akizungumza na HabariLEO, Mratibu na Katibu wa shirika la Environment is Life, Gerald Muunga, amesema miti ina faida nyingi kwa jamii na hivyo wananchi wanapaswa kujenga utamaduni wa kuipanda na kuitunza. “Miti ni tiba, lakini pia hutoa kivuli, husababisha mvua, huzuia mmomonyoko wa ardhi pamoja na mafuriko. Tunapaswa kuwekeza kwenye upandaji miti ili kuhakikisha mazingira yetu yanabaki salama,” amesema Muunga.

Kwa upande wake, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kupitia Ofisi ya Kinondoni, wamehimiza jamii kujitokeza kuchukua miti kwa ajili ya kuipanda kwenye maeneo mbalimbali kama mashuleni, pembezoni mwa barabara na katika taasisi za dini. SOMA: Miti yatajwa kuwa kinga dhidi ya joto kali.

Kanuti Matasha, Askari Mhifadhi Mwandamizi wa Misitu Wilaya ya Kinondoni, amesema: “TFS Kinondoni tupo tayari kutoa miche bure kwa ajili ya kampeni ya upandaji miti. Tunakaribisha mashule, vyuo, na taasisi nyingine kuwasilisha barua zenye kuainisha idadi ya miche na eneo ilipotengwa kwa upandaji.”

Amesisitiza kuwa utunzaji wa mazingira ni jukumu la kila mwananchi na ushirikiano wa pamoja ndio utakaosaidia kudhibiti uharibifu wa mazingira nchini. “Utunzaji wa mazingira unaanza na mimi, wewe na yule. Sote tunapaswa kuchukua hatua sasa,” amehitimisha Matasha.

 

Habari Zifananazo

4 Comments

  1. I get paid more than $100 to $500 per hour for working online. I heard about this job 3 months ago and after joining this I have earned easily 💵$20k from this without having online working skills . Simply give it a shot on the accompanying site…

    Here is I started.………… https://Www.Works6.Com

  2. I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
    .
    HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

  3. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  4. I’m currently generating over $35,100 a month thanks to one small internet job, therefore I really like your work! I am aware that with a beginning cdx05 capital of $28,800, you are cdx06 presently making a sizeable quantity of money online……… https://cashprofit7.site

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button