Korosho Marathon yaja kwa watoto, wazee

BODI ya Korosho Tanzania (CBT) kwa kushirikiana na Kampuni ya Rhino Sports Talents Promotion imezindua vifaa vya mbio za Korosho Marathon msimu wa nne, huku mwaka huu zikitarajiwa kuwahusisha pia watoto na wazee. Mbio hizo zinatarajiwa kufanyika Novemba 29, 2025 mkoani Mtwara, zikiwa na lengo la kutangaza fursa katika tasnia ya korosho, kuhamasisha ulaji wa korosho na kuongeza thamani ya zao hilo.

Mkurugenzi wa Masoko na Udhibiti Ubora wa CBT, Revelian Ngaiza, amesema mbali na mbio za kilomita 5, 10 na 21, mwaka huu kutakuwa na mbio maalumu za kilomita 2.5 kwa watoto wenye umri wa miaka 6 hadi 13, na kilomita 3 kwa wazee wenye umri wa miaka 60 hadi 95. “Tunapanua wigo wa ushiriki ili kujenga kizazi kinachothamini afya na michezo, sambamba na kuimarisha uelewa kuhusu zao la korosho,” alisema Ngaiza.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala, amepongeza waandaaji wa mbio hizo na kuwataka wadau, wawekezaji na wazazi kujitokeza kushiriki, akisema ni fursa nzuri ya kuimarisha umoja na afya kwa jamii. “Ni jambo zuri kuona wazee na watoto wakihusishwa.

Kwa upande wake, Mratibu wa mbio hizo kutoka Rhino Sports, Nelson Mrashan, amewataka wazazi kusajili watoto wao ili kuwajenga katika misingi ya riadha tangu utotoni. “Riadha inaanzia chini. Tunataka kupata wakimbiaji watakaofikia viwango vya kimataifa,” alisema Mrashan. SOMA: Geay atakiwa kuibeba Tanzania riadha Berlin

Msemaji wa mbio hizo, Mohammed Kemkem, amesema zaidi ya washiriki 3,000 wanatarajiwa kushiriki mwaka huu, na kabla ya mbio hizo kutakuwa na Maonyesho ya Korosho yatakayofanyika kuanzia Novemba 24 hadi 28, yakionyesha shughuli na bidhaa zinazohusiana na zao hilo.

 

 

Habari Zifananazo

4 Comments

  1. I have just received my 3rd payment order and $30,000 that I have built up on my laptop in a month through an online agent…!v76) This job is good and his regular salary is much better than my normal job. Work now and start making money online yourself.
    Go here….… https://Www.Smartpay1.site

  2. I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
    .
    HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

  3. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us →→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  4. Nowadays earning money online is very easy . Eanrs every month online more than $17k by doing very easy home based job in part time u can also do this simple online Job by visiting websiteMore Details For Us→→  http://www.job40.media

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button