Rais Mwinyi awateua makatibu wakuu

ZANZIBAR : RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amefanya uteuzi wa makatibu wakuu na manaibu makatibu wakuu wapya wa Wizara mbalimbali za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Said imesema kuwa Fatma Mabrouk Khamis ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano Teknolojia ya Habari na Ubunifu,Khamis Suleiman Mwalimu ameteuliwa kuwa KatibuMkuu Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Dk habiba Hassan Omar ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda.
Wengine walioteuliwa ni Dk Rahma Salim Mahfoudh kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango , Salama Mbarouk Khatib yeye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Vijana Ajira na Uwezeshaji .
Rais Mwinyi pia amemteua Mattar Zahor Masoud kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Saleh Mohammed Juma atakuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo , Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Mhandisi Ali said Bakari akipangiwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. SOMA: Omolo Katibu Mkuu Wizara ya Vijana, Dk Mapana Naibu
Katika uteuzi huu umeambatana sambamba na uteuzi wa manaibu makatibu wakuu ambapo Rashid Ali Salum ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kazi na Uwekezaji, Makame Machano Haji akiwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari , Sanaa , Utamaduni na Michezo.
Wengine Khalid Masoud Waziri akipangiwa Wizata ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji na Mohammed Dhamir Kombo akipelekwa Wizara ya kilimo , Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo na Amosi John Hennock akienda Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali.
Hatahivyo katika uteuzi huo Rais Dk Mwinyi ameamua kuwaacha Makatibu Wakuu kumi na mbili katika Wizara zao kadhalika na Manaibu Makatibu kumi ambao nao wataendelea katika wizara zao za awali .Wateule wote wanatarajia kuapishwa rasmi siku ya Jumamosi wiki hii 22 Novemba katika viwanja vya Ikulu Zanzibar.



