Taasisi yajizatiti mageuzi teknolojia

“Sekta ya teknolojia ni injini ya maendeleo. Tunazitaka kampuni na taasisi mbalimbali kuungana nasi katika kuendeleza juhudi za kulijenga taifa kiteknolojia kwa manufaa ya jamii na uchumi,”.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Dynatech Solutions Limited, Exaud Kimboi ametoa kauli hiyo katika mafunzo maalumu yanayolenga kuleta mageuzi katika teknolojia bunifu, hususan matumizi ya Akili Mnemba ili  kuchochea maendeleo ya sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano.

Amesema kampuni yake imejipambanua kuwa sehemu ya suluhisho la mabadiliko ya teknolojia nchini kwa kutoa elimu inayohitajika ili kujenga mifumo ya kisasa na jengefu.

“Tumeandaa mafunzo haya ili kutoa uelewa mpana kuhusu teknolojia bunifu zitakazochochea ubunifu wa bidhaa madhubuti zenye matumizi mapana ya sayansi ya juu na Akili Mnemba,” amesema Kimboi.

Ameongeza kuwa teknolojia hizo zitasaidia kuboresha na kukuza sekta ya TEHAMA nchini kwa kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo yatakayowezesha uratibu bora wa shughuli za kila siku katika taasisi za fedha, elimu na teknolojia.

Kimboi pia amesisitiza juu ya ushirikiano wa karibu kati ya Dynatech na Serikali kupitia wizara na taasisi mbalimbali, akisema kuwa ushirikiano huo unaonesha namna kampuni hiyo imekuwa chachu muhimu ya mabadiliko ya kiteknolojia nchini.

Amefafanua kuwa Dynatech inaendelea kuwa mshirika mkuu katika kukuza mifumo ya TEHAMA, ikijikita zaidi katika usimamizi wa Cloud Database na uanzishaji wa mifumo mipya ya kisasa.

Kwa upande wake, Meneja wa Dynatech, Wangui Kaboreta, ameeleza umuhimu wa uwepo wa kampuni ya Oracle nchini, akibainisha kuwa kwa zaidi ya miaka 47, Oracle imekuwa ikitoa masuluhisho ya teknolojia kwa taasisi mbalimbali duniani.

Naye Gabriel Mwongera, Principal Senior Engineer wa Oracle, amewasilisha suluhisho jipya la Oracle linalotumia teknolojia ya Akili Mnemba ndani ya mifumo yake, hatua inayoongeza ufanisi katika utunzaji, uchakataji na usimamizi wa taarifa kwa taasisi za kisasa.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  3. Google provides awesome remote work opportunities, allowing me to earn $2000-$3000 weekly with just 2-4 hours of daily work. It’s been a game-changer, offering flexibility and reliable income. If you’re seeking a genuine way to earn online, don’t miss this chance. Start today and transform your life!
    .
    More Details For Us →→ http://www.big.income9.com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button