Mbunge Babati asisitiza amani

MANYARA: Mbunge wa Babati Mji,  Emmanuel Khambay amewataka wananchi wilayani Babati mkoani wa Manyara kulinda amani ya nchi siku zote ili kuishi kwa utulivu kufanya kazi kwa bidii kuinua uchumi wa nchi.

‎Mbunge huyo wa ambaye pia ni mlezi wa maafisa usafirishaji (Bodaboda) amewaonya madereva hao kutofumbia macho viashiria vyovyote ambavyo vinapelekea uvunjifu wa amani kuelekea siku ya kumbukizi ya Uhuru wa nchi  Desemba 9, 2025 na badala yake kutoa taarifa polisi na vyombo vya usalama.

‎Amezungumza hayo katika kikao cha kutoa  elimu kuhusu utunzaji wa amani na utulivu katika nchi kwa maafisa usafirishaji (Bodaboda) wa Wilaya ya Babati katika bwalo la polisi wilayani Babati mkoani Manyara.

‎”Nawasihi endeleeni na kazi zenu za kila siku zinazowaletea riziki katika hali ya  utulivu na mnaposikia viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani ni lazima muwe mstari wa mbele kutoa taarifa polisi na mamlaka husika,” amesema Khambay.

‎Aidha, amepiga marufuku maofisa usafirishaji (Bodaboda) kujihusisha na maandamano yoyote yasiyo rasmi yenye lengo la kuleta vurugu na kuhatarisha amani na utulivu wa nchi.

‎Kamishna msaidizi wa polisi ambaye pia ni Mkuu wa Polisi Jamii mkoa wa Manyara, Kija Mkoyi amewahimiza maafisa usafirishaji kuwa mstari wa mbele katika kutunza amani na kuacha kusikiliza na kushabikia maneno yanayotolewa katika mitandao ya kijamii yanayohamasisha kufanya maandamano ya aina yoyote kufanya vurugu.

‎”Mna wajibu wa kuwa watulivu na kuendelea kufanya kazi za kila siku bila kuwa na hofu kwa kuwa serikali haijatangaza shughuli yoyote ambayo inakusanyisha watu katika mji wa Babati kuelekea siku ya tarehe 9 Disemba 2025 Kuambukizi za uhuru,”amesema.

‎Naye Mrakibu wa Polisi Ernesta Mwambinga, OCD Wilaya ya Babati amesema ni lazima kufuata sheria na taratibu zinazoongoza katika sekta ya usafirishaji ikiwemo usalama barabarani ili kupunguza ajali zinazoweza kuepukika.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button