Akwilapo: Watumishi wasiwe sehemu ya migogoro ya ardhi

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Leonard Akwilapo amesema wizara yake haitaki watumishi wa sekta ya ardhi kuwa sehemu ya migogoro ya ardhi nchini.

Dk Akwilapo alitoa kauli hiyo wilayani Masasi wakati alipowasili na kupokewa kwa mara ya kwanza tangu ateuliwa kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

“Kuanzia sasa hatutaki mtumishi wetu awe sehemu ya tatizo, tukigundua wewe mtumishi wa sekta ya ardhi umekuwa sehemu ya tatizo basi wewe si mfanyakazi wetu na hilo tutalisimamia,” alisema.

Alisema kuwa matatizo ya ardhi yapo na yanatengenezwa na watumishi wa sekta ya ardhi pamoja na wananchi. Ameweka wazi kuwa matatizo yaliyotengenezwa wizara yake itayatatua.

“Hatupendi kufukuza kazi watumishi maana tunajua kila mfanyakazi anategemewa na kumfukuza itakuwa kitu cha mwisho lakini kuna mahali inabidi sheria ifuate mkondo wake,” alisema.

Dk Leonard Akwilapo yupo wilayani Masasi Mkoa wa Mtwara ambapo pamoja na mambo mengine atakutana na wananchi wa jimbo lake kwa lengo la kusikiliza na kizitafutia ufumbuzi changamoto mbalimbali jimboni humo.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. Ni msimu wa sikukuu na tumekusogezea ofa za kibabe na sio za kukosa. Ingia sehemu ya “Offer Zone” kuagiza sasa! https://s.duka.direct/8sxud says:

    6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO

    Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:

    NO PROGRAMME

    1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi

    2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani

    3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni

    4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani

    5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda

    6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu

    7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi

    8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti

    9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini

    10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi

    11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni

    12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini

    13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia

    14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi

  2. ★彡[𝐍𝐄𝐄𝐃 𝐏𝐄𝐎𝐏𝐋𝐄 𝐅𝐎𝐑 𝐏𝐀𝐑𝐓 𝐓𝐈𝐌𝐄 𝐎𝐍𝐋𝐈𝐍𝐄 𝐖𝐎𝐑𝐊]彡★

    Start making cash right now… I get paid over $220 per hour working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my befst friend earns over $19,000 a month doing this and she convinced me to try. ift was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by visiting Following Link…

    𝐇𝐞𝐫𝐞 𝐢𝐬 𝐈 𝐬𝐭𝐚𝐫𝐭𝐞𝐝=========> https://bs786s.blogspot.com/

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button