Amlipa kijana Sh 50,000 amuue mumewe

MOROGORO; Malinyi. JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia Holo Jilia (45), mkazi wa Kijiji cha Kilolero B, Wilaya ya Malinyi , mkoani Morogoro kwa tuhuma za kula njama ya kukodisha kijana na kumlipa ujira wa Sh 50,000 ili akamuue mumewe aitwaye Charles Maghashi (55).
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Alex Mkama amesema hayo Novemba 3, 2023 , kuwa tukio hilo lilitokea Oktoba 29 mwaka huu, ambapo mwanamke huyo na kijana aliyetambuliwa kwa jina la Maela Athanas (33), wote wakazi wa Kijiji cha Kilolero B , wilayani Malinyi wanashikiliwa kwa tuhuma ya mauaji ya Maghashi.
Mkama alieleza sababu kubwa iliyodaiwa kusababisha mauaji ya Maghashi ni ugomvi wa kifamilia baina yao.
“ Kutokana na ugomvi huo …basi mwanamke huyo anadaiwa alikula njama na kufanya hili tukio la mauaji, “ amesema Kamanda na kuongeza kuwa kwa uchunguzi wao Athanas ilikuwa alipwe Sh 900,000, ambapo alitanguliziwa Sh 50,000..
Kwa mujibu wa Kamanda, mtuhumiwa Maela Athanas anadaiwa alikwenda nyumbani kwa marehemu na kumkuta amelala sebuleni kwake na kuanza kumkata sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia kifo chake.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
LiliaHood
LiliaHood
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by LiliaHood
Julia
Julia
1 month ago

Cash generating easy and fast method to work in part time and earn extra $15,000 or even more than this online. By working in my spare time i made $17,000 in my previous month and i am very happy now because of this job.
.
.
Detail Here——————————————————–>>>  http://Www.BizWork1.Com

Back to top button
2
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x