Ashauri kusoma ujasiriamali

MWANAFUNZI Masha Sogoma (65), ameshauri wazee wenzake kusoma elimu ya darasani na ujasiriamali.

Masha ambaye ni mwanafunzi wa elimu ya Mpango wa Uwiano Kati ya Elimu ya Watu Wazima na Jamii (Mukeja), ametoa ushauri huo katika Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima Kitaifa yanayofanyika Kibaha mkoani Pwani.

“Ninawashauri wazee ambao hawajapata hii elimu waingie ili iwasaidie.

“Tumesoma baada ya kusoma tukawezeshwa tujifunze ujasiriamali ili tusikae tu bila kuwa na kitu cha kutuingizia kipato,” amesema.

Ameitaka serikali kuwatambua wazee wengi ambao wako vijiji ambao hawajafikiwa na elimu hiyo.

Amesema baada ya masomo anatengeneza bidhaa za batiki, sabuni, dawa ya kuchua, mafuta ya kupka pamoja na sabuni za mlonge.

Naye Mwalimu wa Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) pamoja na Kisomo chenye Manufaa na Mwendelezo (KCM), Rehema Gabriel amesema ana darasa la wazee kuanzia miaka 60 na kuendelea anaowafundisha katika kituo cha wazee kilichopo Shule ya Msingi Mwendapole A mkoani Pwani.

“Darasa lingine la Kisomo chenye manufaa na mwendelezo linapatikana eneo la CCM Wilaya ya Kibaha,” amesema.

Kwa maelezo yake wanafunzi wake hao wanaingia darasani wanajifunza KKK na stadi za kazi, baadae wanaingia darasani kwa ajili ya ujasiriamali.

Amesema wanafunzi hao wazee wanajifunza kutengeneza bidhaa mbalimbali zikiwemomafuta, sabuni, batiki, mkaa, lishe, sabuni za usafi na nyinginezo nyingi.

Amesema darasa lake la wazee lililopo eneo la Shule ya Msingi Mwendapole A lina wanafunzi 72 ambalo limegawanyika katika madarasa mawili.

“Katika darasa hilo unawabembeleza wazee kama wanafunzi wa chekechea ili waingie darasani, na lile darasa lingine ni la wanafunzi waliosoma zamani ambao sasa tunawakumbushia,” amesema.

Amesema lengo la elimu ya wazee ni kutoa dhana iliyojengeka katika jamii kuwa mtu akishakuwa mzee hana maana.

“Uzee sio kuishia bali ni hazina tunachota hazina za wazee, kule ziliko na kuzileta huku,” alisema na kuongeza kuwa darasa lake lingine lina wazee 30.

Akizungumzia changamoto ameiomba walimu wa madarasa hayo ya wazee wapelekwe mafunzo badala ya kutuia uzoefu katika kufundisha, kwa kuwa mzee ni kama mtoto anahitaji kubembelezwa.

Naye Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Juu, Profesa Michael Ng’umbi amesema wajibu wao ni kuhamasisha jamii kuona elimu ya watu wazima bado ni nyenzo muhimu katika kujenga utu, kuhakikisha kwamba haki ya msingi ya binadamu ya kujua kusoma, kuandika na kuendelea kujifunza muda wote inazingatiwa.

Kwa upande wake Naibu Mkuu wa taasisi hiyo upande wa taaaluma, utafiti na ushauri Dk Philip Sanga amesema elimu hiyo ya watu wazima umuhimu wake ni kukumbusha jamii kuhusu umuhimu wake.

“Elimu ya watoto tunasema inaandaa watoto kwa ajili ya maisha ya baadaye lakini wanapojifunza watu wazima ni kwa aajili ya kujifunza sasa,” amesema.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Work AT Home
Work AT Home
1 month ago

Cash generating easy and fast method to work part time and earn an extra $15,000 or even more than this online. By working in my spare time I made $17990 in my previous month and I am very happy now because of this job. you can try this now by following 

the details here…… http://Www.Smartcash1.com

Last edited 1 month ago by Work AT Home
Royal
1 month ago

Google paid 99 dollars an hour on the internet. Everything I did was basic Οnline w0rk from comfort at hΟme for 5-7 hours per day that I g0t from this office I f0und over the web and they paid me 100 dollars each hour. For more details
visit this article————>> http://Www.SmartCash1.com

Ramonaimmons
Ramonaimmons
1 month ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 1 month ago by Ramonaimmons
Michael Chiarello
Michael Chiarello
1 month ago

Tukifanyikiwa:-

KUTAKUWA NA AKILI ZA

  1. MSHAHARA
  2. MARUPULUPU
  3. FEDHA ZA SAFARI
  4. FEDHA ZA KWENDA KUSOMAKUONGEZA TAALUMA ZA RELI
  5. KILA MTANZANIA ATAPEWA MILIONI 100 ZA KWENDA KUSOMA ULAYA

WAMEGOMA KUWA MCHINGA ANAISHI VIZURI KULIKO MTUMISHI WA UMMA

Back to top button
4
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x