CCM yaahidi kukabili wanyama waharibifu

MOROGORO: MGOMBEA Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel Nchimbi amesema kuwa endapo CCM itapewa ridhaa ya kuongoza tena serikali katika kipindi cha miaka mitano ijayo, itaweka mkazo mkubwa katika kukabili wanyama waharibifu wanaovamia mashamba kwa kutumia teknolojia ya ndege zisizo na rubani, ili kulinda mazao na kuongeza tija kwa wakulima.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kilombero juzi jioni, Dk Nchimbi alisema tayari serikali imeshaanza maandalizi ya mfumo huo utakaotumika kuwafukuza tembo na wanyama wengine waharibifu, kwa kushirikiana na viongozi wa maeneo husika ili kuhakikisha mazao ya wananchi yanabaki salama wakati wote wa uzalishaji.
“Nataka niwahakikishie nitashiriki kuhakikisha mipango ya kutumia ‘drones’ kuwafukuza wanyama waharibifu inatekelezwa. Hii itawasaidia wakulima wetu kuendelea kuzalisha bila hofu, mazao yaongezeke na nchi yetu iendelee kupata maendeleo,” alisema.
Aidha, alibainisha kuwa katika sekta ya kilimo, Serikali ya CCM imepanga kuimarisha zaidi uzalishaji kwa kuanzisha mashamba darasa yatakayowapa mafunzo wakulima kuhusu kilimo cha mazao yenye tija kubwa kama michikichi, ufuta, parachichi na korosho.
JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com