Coco Gauff ampa ‘thank you’ kocha wake

Mcheza tenisi namba sita duniani kutoka Marekani, Coco Gauff, ameachana na kocha wake Brad Gilbert wiki mbili tu baada ya kile alichokitaja kuwa kampeni ya kukatisha tamaa kutetea taji la US Open.

Gauff, 20, alishinda taji lake la kwanza kubwa la mchezo huo jijini New York mwaka uliopita chini ya usimamizi wa Gilbert.

SOMA: Fahamu mashindano makubwa ya tenisi duniani

Lakini amelipoteza mwaka huu katika raundi ya nne kwa Mmarekani mwenzake Emma Navarro.

Gauff alimuajiri Gilbert Julai 20, 2023 kufanya kazi pamoja na kocha wa kihispania Pere Riba baada ya kutolewa raundi ya kwanza ya michuano ya Wimbledon mwaka uliopita.

Habari Zifananazo

Back to top button