DC ataka suluhu changamoto za wakulima wa Tumbaku

MKUU wa Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi Onesmo Buswelu amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya hiyo kuhakikisha anakaa karibu na wakulima kupitia vyama vya ushirika (AMCOS) pamoja na Afisa ushirika ili kujua changamoto zinazo wakabili wakulima.

Ametoa maagizo hayo katika Mkutano Mkuu wa wakulima wa Tumbaku uliofanyika Kijiji cha Ifukutwa Kata ya Mpanda Ndogo wilayani humo,baada ya wakulima kuwasilisha malalamiko yao kuwa wapo baadhi ya mawakala ambao wanakataa kuwauzia mbolea aina ya NPK.

“Msamahazaji wa mbolea ambaye anafahamu utaratibu halafu anakataa kuuza NPK, kwa hakika serikali itachukua hatua kali kwake”amesema na kuongeza

“Taarifa ikitufikia usiku tunafanya kazi usiku huo huo,zikifika asubuhi tunafanya kazi asubuhi hiyo hiyo, hatuchelewi kwenye suala la kilimo kwa sababu kilimo ndiyo uchumi wa nchi yetu”

Hatua hiyo imemlazimu kutoa mawasiliano yake ya simu ya mkononi kwa wakulima hao ili waweze kumfikishia malalamiko yao moja kwa moja kuhusu changamoto wanazokumbana nazo za upatikanaji wa mbolea.

Hata hivyo,aliwataka wakulima wapatao elfu sitini walio salia kujiandikisha kwenye mfumo wa upataji mbolea ya ruzuku kujitokeza ili waweze kupata mbolea hiyo badala ya kulalamika.

Kwa upamde wake Mrajisi Msaidizi wa vyama vya msingi Mkoa wa Katavi Peter Nyakunga aliwaonya wanachama au viongozi wa vyama vya msingi wanao vuruga vyama lengo vivunjike na kisha waanzishe vyama vyao kwa tamaa za madaraka.

Awali, baadhi ya wakulima walilalamika kutofikiwa na pembejeo maeneo ya vijijini huku akihoji uwepo wa mbolea ya NPK kwenye ruzuku.

 

Habari Zifananazo

13 Comments

  1. 661722 257569I discovered your blog website internet site on the search engines and check several of your early posts. Always preserve up the extremely good operate. I lately additional increase Rss to my MSN News Reader. Seeking for toward reading a lot far more on your part later on! 183913

  2. 815336 360223An fascinating discussion might be worth comment. I think you need to write on this topic, it might definitely be a taboo topic but usually people are not enough to dicuss on such topics. To a higher. Cheers 353122

  3. 555156 461487 An fascinating discussion is worth comment. I think which you should write much more on this subject, it may possibly not be a taboo subject but generally folks are not enough to speak on such topics. Towards the next. Cheers 878221

  4. 309037 139746Your blog is one of the far better blogs Ive came across in months. Thank you for your posts and all the greatest with your work and blog. Looking forward to reading new entries! 855111

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button