Dk.Kijaji aitaka TTB kuongeza nguvu katika utafiti,masoko

SERIKALI kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeitaka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kuongeza nguvu katika utafiti na masoko ya bidhaa za utalii ili kufikia lengo la kuileta Tanzania kwenye idadi ya watalii milioni nane, kama ilivyoainishwa katika Ilani ya CCM ya mwaka 2025–2030.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya kikazi alipotembelea ofisi za TTB jijini Dar es Salaam. Dk. Kijaji amesema kuwa ni muhimu kubadili mifumo ya kuyafikia masoko ya kimataifa ili kuvutia watalii wengi zaidi kuja nchini.

“Jambo kubwa tulilokubaliana ni kubadilisha namna tunavyoyafikia masoko ya nje ili kuwafikia wateja tunaowalenga na kuhakikisha wanakuja nchini. Hii itatusaidia kutimiza malengo ya watalii milioni nane ndani ya miaka mitano ijayo,” alisema.

Aidha, Waziri Kijaji alisisitiza umuhimu wa kuboresha bidhaa za utalii ili kuhakikisha watalii wanaofika nchini wanavutiwa na kurejea, sambamba na kuwashawishi wengine kuitembelea Tanzania, hatua itakayoongeza pato la Taifa. SOMA: ‘TTB tumieni AFCON 2027 kuongeza watalii’

Katika hatua nyingine, ameielekeza TTB kuongeza nguvu katika utafiti ili kubaini vivutio ambavyo bado havijafika sokoni, maeneo vilipo, pamoja na kufanya kazi kwa karibu na taasisi zinazomiliki rasilimali hizo.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button