East Africa Golf Tour kuanza Agosti

DAR-ES-SALAAM: Shindano la wazi la Mchezo wa Gofu”KCB  East Africa Golf Tour” Linatarajiwa kufanyika Agosti 3 katika Klabu ya Jeshi La Ulinzi La Wananchi Wa Tanzania-JWTZ  Lugalo Gofu jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Wanahabari  Leo Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo Mwenyekiti wa Klabu ya Gofu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania-JWTZ Lugalo Gofu amesema, shindano nila siku moja linatarajia kupata wawakirishi watakoecheza finali.

“Shindano ni la siku moja huku likiwa na lengo la kupata Wachezaji wanne watakaoiwakilisha nchi kwenye Fainali za Michuano hiyo nchini Kenya.”amesema Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo (Mwenyekiti Lugalo Gofu)

Advertisement

Kwa Upande wake Meja Japhet Masai Nahodha wa Lugalo Gofu amesema, Shindano Hilo litachezwa Kwa Mfumo wa Kimataifa wa  “Stable Ford” ambapo Mshindi atapatikana Kwa kuhesabu Alama kwenye Kila shimo.

Naye  Mkurugenzi Mkuu wa KCB Bank Tanzania  Cosmos Kimario amesema, shindano Hilo litakuwa likifanyika Kila Mwaka huku lengo likiwa ni kuendeleza Michezo nchini hasa Mchezo wa Gofu.

SOMA: Lugalo Golf Fundraiser’ kusisimua gofu kwa watoto

Shindano la “KCB  East Africa Tour” Linatarajiwa kufanyika Agosti 3,2024 likiwa na lengo la kutafuta Wachezaji wanne watakao iwakikisha nchi kwenye Fainali nchini Kenya.

SOMAhttps://www.bbc.com/swahili/michezo/2015/04/150427_tanzania_golftournament