HAITI : Marekani yalaani mauaji vikongwe 180

HAITI : MAREKANI imelaani  vikali mauaji ya watu 200 ambayo yanadaiwa kufanywa na wanachama wa magenge ya uhalifu nchini Haiti.

Msemaji wa ikulu ya Marekani, Karine Jean-Pierre amesema kuwa ripoti  hiyo imeishtusha Marekani.

Mwanzoni mwa wiki hii , Ofisi ya waziri mkuu wa Haiti ilidai kuwa watu 180 ambao vikongwe waliuawa katika eneo la Cite Soleil baada ya kushambuliwa. SOMA: Watu 70 wamekufa Haiti

Advertisement

Shirika moja lisilo la kiserikali lilisema kuwa mashambulizi hayo yalifanywa na kiongozi mmoja wa genge la uhalifu ambaye anadaiwa  mwanawe kufanyiwa  mambo ya kishirikina.