Hemed ateuliwa tena Makamu wa Pili

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amemteua tena Hemed Suleiman Abdulla kuwa Makamu wa Pili wa Urais Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Zena Saidi, imeeleza kuwa uteuzi huo umeanza rasmi leo, Novemba 6, 2025. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Hemed anatarajiwa kuapishwa Jumamosi, Novemba 8, 2025, saa nne asubuhi katika viwanja vya Ikulu Zanzibar.

Uteuzi huo unaendeleza imani ya Rais Dk. Mwinyi kwa kiongozi huyo ambaye amehudumu katika nafasi hiyo tangu awamu iliyopita. SOMA: Zuberi Maulid ashinda kwa kishindo Spika Baraza la Wawakilishi

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button