Jimmy Carter kuzikwa 9 Januari 2025

MAREKANI : MAZISHI ya kitaifa ya Rais wa zamani wa Marekani, Jimmy Carter yatafanyika katika Kanisa Kuu la katoliki mjini Washington Januari 9 .

Kwa mujibu wa taarifa  iliyotolewa Ikulu ya White house imesema  kuwa  Januari 9 itakuwa siku maalum ya maombolezo ya kitaifa ya Jimmy Carter.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa  siku sita za mazishi ya kitaifa  zitaanza  jumamosi wiki hii hadi tarehe 9 Januari ambapo atazikwa.

Jeshi nchini Marekani limesema mwili wake utasafirishwa kwa msafara wa magari kupitia mji aliozaliwa wa Plains katika jimbo la  Georgia. SOMA : Rais wa zamani wa Marekani Jimmy Carter amefariki dunia

Msafara huo  pia utasimama shambani alikokulia, kisha mwili wa Carter utasafirishwa hadi Atlanta, ambako utalala katika Kituo cha Carter hadi asubuhi ya Januari 7.

Kisha baadae mwili utasafirishwa hadi Washington, DC ambako utalazwa katika majengo ya Bunge la Marekani – Capitol Hill hadi pale itakapofanyika ibada ya kitaifa ya kuuaga.

Jimmy Carter amepangwa  kuzikwa Georgia Januari 9 pembezoni mwa  kaburi  la mke wake, Rosalynn Carter ambaye amezikwa nyumbani kwao mjini Plains.

Carter  alifariki dunia  mwishoni mwa wiki hii baada ya kusumbuliwa na maradhi ya muda mrefu na amefariki akiwa na umri wa miaka 100.

Habari Zifananazo

Back to top button