JK: Wamesahau, au wanajifanya hamnazo!

DAR ES SALAAM; RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk Jakaya Kikwete, amesema baadhi ya watu wanaodai utaratibu umekiukwa wa kumpata mgombea urais wa CCM kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu pengine wanajifanya hamnazo.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za CCM jijini Dar es Salaam leo Agosti 28, Kikwete amesema wanaopinga utaratibu wa kumpata Dk Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea urais wa CCM pengine hawafahamu utaratibu wa CCM.
“Na kama wanafahamu labda wamesahau au wanajifanya hamnazo,” amesema Kikwete.



