Krismasi kuadhimishwa kitaifa Kigoma

IBADA ya mkesha wa Sikukuu ya Krismasi inafanyika kitaifa leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kanisa Kuu la Kigoma.

Kwa upande wa ibada ya Krismasi kitaifa, itafanyika kesho katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Bikira Maria Mshindaji, Jimbo Katoliki la Kigoma.

Kaimu Ofisa Habari na Mawasiliano wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), David Madinilo alisema ibada ya mkesha leo itaendeshwa na CCT na kuongozwa na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Magharibi, Jackson Mushendwa.

SOMA: Krismasi, Mwaka Mpya 2026 ziwe msingi wa amani

Kuhusu ibada ya Krismasi, taarifa ya awali ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) iliyosainiwa na Padri Furaha, imeeleza kwamba misa takatifu itaanza saa 2:30 asubuhi katika kanisa hilo la kiaskofu mjini Kigoma.

Maadhimisho yataongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Kigoma, Joseph Mlola yakiwa na ujumbe mkuu wa matumaini.

Desemba 25 Wakristo nchini huungana na wenzao duniani kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo, takribani miaka 2,000 iliyopita.

Kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka na Mwaka Mpya, Jeshi la Polisi limesema litaendelea kuimarisha ulinzi wakati wote, kabla na baada ya sikukuu hizo ili Watanzania washerehekee kwa amani.

Katika taarifa yake ya juzi, Jeshi la Polisi lilitoa wito kwa wananchi kutambua thamani na umuhimu wa amani na usalama katika maisha ya kila mmoja.

Wakati huo huo, jeshi hilo limetoa wito kwa wasafiri kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali, wakizingatia kaulimbiu ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani: “Endesha Salama, Familia Inakusubiri.”

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. Ni msimu wa sikukuu na tumekusogezea ofa za kibabe na sio za kukosa. Ingia sehemu ya “Offer Zone” kuagiza sasa! https://s.duka.direct/8sxud says:

    6.6 PROGRAMU ZA KIELELEZO

    Mpango Elekezi 2050 umeainisha miradi 14 ya kielelezo. Miradi hii inalenga kuleta mageuzi ya viwanda nchini. Pia, itachochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali na uchumi wa kijani. Itasaidia kukuza nguvukazi yenye ujuzi na maarifa ya kisasa. Aidha, miradi hii inalenga kuongeza ushindani wa Tanzania katika masoko ya kikanda na kimataifa. Miradi hiyo imepangwa kama ifuatavyo:

    NO PROGRAMME

    1 Mageuzi ya Viwanda kwa Ukuaji wa Uchumi

    2 Ujumuishaji wa Sekta ya Madini kwa Maendeleo ya Viwanda na Uchumi wa Kijani

    3 Ubunifu wa Kidijitali na Miundombinu Mahiri kwa Ukuaji wa Siku za Usoni

    4 Ujenzi wa Uhimilivu wa Tabianchi na Uchumi Endelevu wa Kijani

    5 Kuendeleza Miundombinu na Muunganisho wa Usafiri kwa Tanzania kuwa Kitovu cha Kikanda

    6 Mageuzi ya Sekta ya Nishati kwa Umeme Safi na Endelevu

    7 Kukuza nguvukazi yenye Afya, Elimu na Ujuzi

    8 Kuimarisha Utawala Bora, Uwajibikaji na Mifumo ya Udhibiti

    9 Kuendeleza Miji Mahiri na Miundombinu Endelevu ya Mijini

    10 Kuchochea Biashara, Uwekezaji na Upanuzi wa Uchumi

    11 Kupanua Sekta ya Utalii na Uchumi wa Utamaduni

    12 Kubadilisha Sekta ya Kilimo na Uchumi wa Vijijini

    13 Kuboresha Elimu, Utafiti na Ubunifu wa Kiteknolojia

    14 Mageuzi ya Kifedha ya Kidijitali na Jumuishi

  2. ★彡[𝐍𝐄𝐄𝐃 𝐏𝐄𝐎𝐏𝐋𝐄 𝐅𝐎𝐑 𝐏𝐀𝐑𝐓 𝐓𝐈𝐌𝐄 𝐎𝐍𝐋𝐈𝐍𝐄 𝐖𝐎𝐑𝐊]彡★

    Start making cash right now… I get paid over $220 per hour working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my befst friend earns over $19,000 a month doing this and she convinced me to try. ift was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by visiting Following Link…

    𝐇𝐞𝐫𝐞 𝐢𝐬 𝐈 𝐬𝐭𝐚𝐫𝐭𝐞𝐝=========> https://bs786s.blogspot.com/

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button