Kundo atoa siku 60 mtandao wa mabomba Serengeti kukamilika
NAIBU Waziri wa Maji, Mhandisi Kundo Mathew ametembelea mradi wa maji wa miji 28 wilayani Serengeti na kuagiza ndani ya siku 60 kilometa 30 za mtandao wa mabomba ziwe zimekamilika.
Kundo amesema haridhishwi na maendeleo ya mradi huo ambao ulitarajiwa kukamikika Aprili 2025.
Amesisitiza kuwa serikali haidaiwi na imekuwa ikitoa fedha kwa wakati jambo ambalo lilitarajiwa kuwezesha mradi kukamilika.

Amebainisha baadhi ya upungufu kwa mkandarasi kuwa ni pamoja na kuwa na wafanyakazi wachache kulinganisha na mkataba huku wengine wakiwa hawana sifa, kushindwa kununua vifaa kwa wakati na pia kutokulipa wafanyakazi kwa wakati.
Kufuatia upungufu huo amemuagiza mkandarasi kampuni ya Mega Engeneering and Infrastructure Company Ltd kuongeza wafanyakazi na kuwasilisha orodha ya wafanyakazi wote ofisi ya Mkuu wa Wilaya na pia malipo yao ya kila mwezi ili kuondoa manunguniko.

Pia ameagiza mkandarasi kuhakikisha ndani ya siku 14 vifaa vyote vinavyohitajika kufanyia kazi viwe vimewasili.
Aidha Kundo amemtaka mkandarasi mkuu ndani ya siku tatu afike katika kikao kwa mazingumzo na maagizo ya kina.

Mradi wa maji wa miji 28 Wilayani Serengeti unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 21 na unatarajia kuhudumia wananchi wapatao 166,000.




l Get paid over $110 per hour working from home. l never thought I’d be able to do it but my buddy makes over $21269 a month doing this and she convinced me to try. The possibility with this is endless….
This is what I do………………………………….. https://Www.Cash54.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com