Mashujaa wetu sasa kurejea Alhamisi asubuhi

DAR ES SALAAM; TIMU ya Taifa ya mpira wa miguu ya (Taifa Stars), ambayo ilikuwa irejee nchini Jumatano Januari 7, 2026, sasa itarejea Alhamisi Januari 8, 2026.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema mabadiliko hayo yana lengo la kuiwezesha timu hiyo kuwasili muda mzuri ambao utatoa nafasi kwa Watanzania kuwapokea na kuwapongeza wachezaji kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya wakiwa katika mashindano AFCON2025 yanayoendelea nchini Morocco.

Msigwa amesema timu itawasili siku hiyo saa 4 asubuhi na itapokelewa na wananchi wakiongozwa na Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi.

Msigwa ametoa wito kwa wananchi wa Dar es Salaam kujitokeza kuwashangilia na kuwapongeza mashujaa hao kwa kazi kubwa na nzuri waliyoifanya nchini Morocco.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. l Get paid over $110 per hour working from home. l never thought I’d be able to do it but my buddy makes over $21269 a month doing this and she convinced me to try. The possibility with this is endless….

    This is what I do………………………………….. https://Www.Cash54.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→→→→→→→ https://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button