Miss Universe Somalia ameacha somo mashindano ya urembo

DAR-ES-SALAAM : UTAMADUNI wa Kisomali unamuongoza  mwanamke wa Kisomali kama  mtu wa kipekee ambaye jukumu lake ni uangalizi wa familia na uzalishaji, nikimaanisha usimamizi wa mifugo na kuongeza  familia.

Mfumo dume umetawala  karne na karne katika familia za Kisomali, ambapo mwanamke hana uwezo wa kufanya kitu sawa na mwanaume, huku wakifuata zaidi na miongozi ya kidini.

Hapo mwanzo walikuwa wanatumiwa  kama  vyanzo vya mtaji kwa jamii  inayowazunguka, lakini ndoa zao zilianza kubadilika baada ya wanawake hawa wa kisomali kuolewa na jamii zingine tofauti.

Advertisement

Ingawa tamaduni za kibaba zilikuwa zinatawala na kutambua majukumu yao hasa kama wake na mama, wanawake wa Kisomali walitumia tamaduni hizo pamoja na rasilimali za kienyeji zilizokuwapo kuweza kufanya maamuzi, kujadiliana nafasi zao, na kuunda maeneo yao binafsi.

Kuletwa kwa utawala wa kikoloni, kuligawanya wasomali kati ya Uingereza, Ufaransa, Italia, na himaya ya Ethiopia, kulileta mabadiliko makubwa katika maisha ya wanawake.

Kulileta muunganiko wa uhusiano wa kibaba na uhusiano wa Kiebrania, kuandika sheria za jadi na kutambulika kwa majukumu ya jamii, na kuwafanya wanawake kama wategemezi wa jamaa zao za kiume, huku likiunda fursa za kimasomo na ajira kwa wanaume, ambazo hazikuwapo kwa wanawake.

Ingawa wanawake wa Kisomali walikuwa mstari wa mbele katika harakati za kupinga ukoloni, kundi la wanaume wa tabaka la juu waliorithi utawala baada ya uhuru walizuwia wanawake kuingia kwenye siasa.

Haki za wanawake zilichukua nafasi muhimu katika utawala wa kijeshi wa Jenerali Mohamed Siad Barre, lakini ukandamizaji na ukatili wa kifedha ulioambatana na utawala wake ulishuhudia athari kubwa kwa wanawake.

Vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyofuatia baada ya kuvunjika kwa serikali ya Kisomali vimeathiri wanawake kwa karibu.

Mbali na uzoefu wa  ukatili wa kijinsia, hali ya kihafidhina ya jamii ya Kisomali imefanya  kupotea kwa mafanikio mengi yaliyopatikana kwa haki za wanawake baada ya uhuru.

Kutoka kwa jamii ya kabla ya ukoloni, utawala wa kikoloni, utawala wa kijeshi, na vita vya wenyewe kwa wenyewe, wanawake wa Kisomali wameonesha uthubutu wa uwezo wao wa kufanya maamuzi , na nguvu ya kuleta mabadiliko hata katika hali ngumu za maisha.

Khadija Omar ni msichana mwenye umri wa miaka 23, ambaye  ameonesha  mfano kwa jamii ya Kisomali na jamii ya Kiislamu  katika mashindano ya  dunia ya ulimbwende Miss Universe 2024, amekabidhiwa taji la Miss Universe  2024  katika ukanda wa Afrika.

Ushiriki wake  umetengeneza historia  kubwa na ya kipekee kama mwanamke wa kwanza kuvaa hijabu kuwakilisha nchi yake katika mashindano ya Miss Universe yenye heshima kubwa duniani.

Mrembo huyu alizaliwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Hagadera nchini Kenya, na safari ya Khadija kutoka mkimbizi hadi kuwa mshiriki wa mashindano ya urembo ya kimataifa ni ya kipekee.

Yeye pia ni Miss Universe Somalia wa kwanza kushiriki katika kiwango hiki, akianzisha hatua mpya kwa taifa la Somalia. SOMA : Miss Universe Afrika Kusini avuliwa uraia

Mnamo mwaka 2010, Mrembo Khadija na familia yake walihamia nchini Kanada, ambapo alipata mabadiliko  makubwa ambayo yalichangia katika kuunda mwelekeo  mpya wa maisha yake.

Kukulia katika nchi mpya kulimwezesha kukumbatia mizizi yake ya Kisomali, huku akikutana na fursa na changamoto za mazingira tofauti ya mila na desturi.

Uzoefu wake wa mitindo na urembo ulimfanya  Khadija kuwa na shauku  kubwa ya kuwakilisha wanawake wa Kisomali na wanawake Waislamu duniani kote, ambapo viwango vya uzuri na utofauti bado vinabadilika.

Ushiriki wa Khadija katika Miss Universe unawakilisha zaidi ya uzuri; unasimamia ustahamilivu wa wanawake wa Kisomali na jamii kubwa ya Waislamu.

Wakati katika amshindano haya  mrembo Khadija  alishiriki akiwa amevaa hijabu, Khadija anataka kupinga dhana potofu na kubadilisha mifumo …