Mwaitege akanusha uzushi wa kifo

DAR-ES-SALAAM: Mwimbaji wa Nyimbo za Injili nchini,Boniface Mwaitege  amekanusha taarifa zinazosambazwa katika mitandao ya kijamii kuwa yeye amefariki.

Akikanusha taarifa hiyo kwenye  mitandao ya kijamii, Mwaitege amesema anashangaa  kuona watu wanaandika  taarifa  ambazo sio sahihi  na kudai kuwa yeye mzima na wala hajafariki.

Pia amewaomba mashabiki  wake kupuuzia taarifa hiyo ambayo   haina ukweli   wowote  bali ni kuchafuana kwenye  mitandao  ya kijamii ama wanataka kupata  wafuasi wengi kweney mitandao yao.

Advertisement

“ndugu zangu mnaonitazama niko mzima, mwenye   afya kama mnavyoniona  sijapata ajali yoyote  sina tatizo  lolote  ni uzushi tu kwahiyo naomba kama unanisikia  nisaidie kufikisha taarifa  hii kwa wengine ili kujaribu kushusha  presha ya uzushi huu ambayo bado sijajua chanzo nini”, alisema  Mwaitege