Oscar apewa mwongozo wa maadili

DAR-ES-SALAAM : MSANII na mwanahabari maarufu, OscarOscar, amepewa Mwongozo wa Maadili katika Kazi za Sanaa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kufuatia mjadala ulioibuka kuhusu wimbo wake mpya, “Mniombee”, ambao umetafsiriwa na baadhi ya wadau kuwa hauna maadili.

Katika kikao kilichofanyika kwenye ofisi za BASATA jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Dkt. Kedmon Mapana, alimkabidhi Oscar mwongozo huo na kusisitiza wajibu wa wasanii kuzingatia maadili na weledi wanapotekeleza kazi zao za kisanaa.

“Wasanii wanapaswa kutumia Mwongozo huu kama rejea ya kila siku ili kuhakikisha kazi zao zinaakisi maadili ya Kitanzania,” amesema Dkt. Mapana.

Pia ameongeza kuwa wimbo wa Osca Osca unaruhusiwa kupigwa usiku kuanzia saa 6 watoto wakiwa wamelala na sio mchana. Tukio hili limejiri siku moja tu baada ya Oscar kunukuliwa na vyombo vya habari akisema, “hip hop ya Tanzania haina maudhui, nimekuja kuirudisha,” kauli iliyozua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari.

Oscar anatarajiwa kuwa mfano wa msanii anayeendeleza ubunifu, ujumbe wenye maudhui, na kuzingatia misingi ya maadili katika kazi za sanaa, huku wadau wakisubiri kwa hamu kuona mwelekeo mpya atakaochukua.

SOMA: Basata yamfungia Babu wa Tiktok

Habari Zifananazo

One Comment

  1. Single Mom Reveals How She Earns $89k/Yr Working 10 Hrs/Week From Home. Tired of paycheck-to-paycheck living? Meet Kelly from New York—a regular mom who cracked the code to recession-proof income without selling a thing! Now, YOU can too with the Home Profit System:

    ACT NOW➢ https://Www.Earnapp1.com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button