Rais Salva Kiir awafuta kazi mawaziri wawili

RAIS wa Sudan Kusini, Salva Kiir amewafuta kazi mawaziri wawili na gavana wa jimbo la Warrap kaskazini mwa nchi hiyo.

Kiir alimfukuza kazi Waziri wa Maswala ya Rais, Barnaba Marial Benjamin, pamoja na Waziri wa Biashara, Kuol Athian.

Pia alimuondoa Waziri wa Utumishi wa Umma, Bangasi Joseph Bakosoro na kumfanya Waziri wa Masuala ya Rais.

Hakuna sababu iliyotolewa ya kufutwa kazi, lakini ni kufuatia kutimuliwa hivi karibuni kwa maofisa kadhaa wa usalama ikiwa ni pamoja na mkuu wa polisi kutokana na uvumi wa mapinduzi.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button