Sh milioni 450 kutengeneza madawati Morogoro

HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro imetenga Sh milioni 450 katika mwaka wa fedha  2023/2024 ili  kutengeneza madawati ya wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ukiwa mkakati wa kuondokana na upungufu wa madawati.

Mkurugenzi wa Manispaa hiyo , Ally  Machela amesema hayo mbele ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Morogoro Mjini, Kichama Fikiri Juma wakati wa ziara ya kamati yake ya  siasa ya wilaya kukagua miradi ya maendeleo na kusikiliza changamoto za utekelezaji wake.

Machela amelazimika  kutoa maelezo hayo wakati kamati hiyo ilipotembelea shule ya msingi Lugala iliyopo kata ya Mindu ambayo alijionea upungufu mkubwa madawati  na kuwafanya  baadhi ya wanafunzi kukaa chini sakafu.

“Kwa mwaka huu wa fedha tumetenga zaidi ya Sh milioni 450 kwa ajili ya utengenezaji wa madawati ili kuondoa adha ya watoto kukaa chini , kwa shule za msingi  tumetenga Sh milioni  250 na  kwa shule za sekondari sh milioni 150  na hii yote ni kwa ajili ya kuondoa adha ya upungufu wa madawati shuleni “ amesema  Machela

Amesema  kwa sasa  wapo katika  mazungumzo  na Uongozi wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) ambacho kinamiliki  kiwanda  cha  kisasa cha kutengeneza  samani waweze kutengeneza   madawati  kwa  matumizi ya wanafunzi wa shule za Manispaa .

Naye Mwalimu mkuu wa shule ya Lugala, Weba Komba amesema  kuwa shule hiyo wenye wanafunzi 881 ina madawati 150 na upungufu  ni 121 kuanzia  darasa la kwanza hadi la saba .

Mwalimu Komba amesema shule hiyo ilianzishwa kwa nguvu za wananchi na baadaye uongozi wa halmashauri  ukaongeza fedha za  kumalizia ujenzi hiyo  ambayo kwa sasa inatumika .

Mmoja wa  mzazi  wa mwanafunzi wa  shule hiyo, Agnes Chitila amesema kukaa chini kwa wanafunzi hasa wa madarasa ya awali  wamekuwa wakichafua nguo  zao  hali inayowalazimu wazazi kutumia kiasi kikubwa cha fedha  kununua maji ya kufulia nguo za zao kila siku .

“Mtoto akirudi nyumbani amechafuka  kila siku ni kufuaa nguo za shule wakati  maji hatuna , tununua dumu la lita ishirini Sh  500 mbali na gharama nyingine tunaomba halmashauri iwatengenezee madawati.“ amesema   Chitila

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments
Back to top button
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x