Wafanyabiashara kutozwa kodi ndogo

ZANZIBAR : RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ameaziagiza taasisi zinazosimamia masoko mapya  kuweka viwango  vidogo vya  malipo  kwa  wafanyabiashara na wajasiriamali ili  wamudu  kulipa  na kuendelea na biashara  katika mazingira mazuri.

Rais Dk,Mwinyi alizungumza wakati alipofungua  soko jipya la kisasa la Jumbi, Mkoa wa Mjini Magharibi, Dk.Mwinyi amewahakikishia wafanyabiashara kuwa serikali itaendelea kuwaandalia mazingira bora zaidi yatakayoendana na  soko hilo.

Rais Dk, Mwinyi  amesisitiza kuwa serikali   imetenga kiasi cha shillingi bilioni mia moja kwa ajili ya kuwapatia mitaji wajasiriamali na wafanyabiashara kuimarisha biashara zao .

Advertisement

SOMA: TRA kuwaongezea faida wafanyabiashara

Halikadhalika Rais Dk, Mwinyi  ameruhusu wafanyabishara kufanya shughuli zao muda wote  na kuagiza soko kuwa wazi Usiku na mchana.

Vilevile Rais Dk,Mwinyi amewaahidi wananchi kuwa  ataendelea kujipambanua kwa Vitendo kutimiza ahadi alizoziahidi wakati wa Kampeni  mwaka 2020.