Taifa Stars waoga noti za Samia

RAIS Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi ya kuipatia timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ Sh milioni 10 kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Niger Jana.

Pesa hizo zimewasilishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa wakati wa kuipokea timu baada ya kuwasili leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam.

“Kama mnavyojua Mheshimiwa Rais aliahidi kwamba kwenye safari ya taifa stars kila goli atakuwa anatoa Sh milion 10” amesema Msigwa

Pamoja na hilo Rais Samia amelipia eneo la mzunguko lenye takriban viti 30,000 kwajili ya Watanzania watakao fika kuishangilia timu ya taifa siku ya jumanne Novemba 21 kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa ikiwa ni sehemu ya kampeni maalum iitwayo “oparesheni Samia Kombe la Dunia” kwajili ya kuhamasisha timu Kushiriki kombe la dunia.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
MONEY MARKER
MONEY MARKER
18 days ago

Mbunge wa KWANZA MZUNGU KWENYE BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA… KUWAKILISHA HELA ZA WORD BANK, IMF, MISAADA KUTOKA ULAYA… N.K – ZA KUJENGEA BARABARA, RELI, FLYOVER,

file:///C:/Users/User/AppData/Local/Temp/msohtmlclip1/01/clip_image002.jpg

HELA ZAO HAZINA MWAKILISHI – KAMA FUNDI ANAHITAJI NYUMBA YAKE KWA SABABU ALIJENGA YEYE (MCHANGA KANIPA HELA)

Back to top button
1
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x