Wawili wakamatwa wakisafirisha dawa za kulevya

ARUSHA: Jeshi la Polisi mkoani Arusha limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 188 kwa makosa mbalimbali ikiwemo ya wizi na usafirishaji wa dawa za kulevya ambapo kati yao, wawili wamekamatwa na bunda 542 za madawa ya kulevya yadhaniwayo kuwa ni mirungi yenye uzito wa kilo 298.
Akitoa taarifa hiyo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Salvas Makweli leo Novemba 14, 2023 amesema Jeshi hilo lilifanya operesheni maalumu kuanzia Oktoba 13, 2023 hadi Novemba 13, 2023 kwa lengo la kuwakamata watuhumiwa wanaojihusisha na matukio ya uhalifu na kufanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao.
ACP Makweli amebainisha kuwa Novemba 12, 2023 muda wa saa 03:00 asubuhi huko katika maeneo ya Philips katika Halmashauri ya Jiji la Arusha walifanikiwa kumkamata Gilbert Joseph (33) mkazi wa Sinoni Jijini Arusha na Peter Waweru (33) mkazi wa nchi jirani wakiwa wanasafirisha madawa ya kulevya yadhaniwayo kuwa ni mirungi bunda 542 yenye uzito wa kilogramu 298, kwa kutumia gari aina ya Isuzu (namba zimehifadhiwa).
Aidha amesema watuhumiwa wote wawili wanaendelea kuhojiwa, pindi upelelezi utakapokamilika jalada litapelekwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Jeshi la Polisi mkoani humo linawaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha limewataka watu wachache wanaojihusisha na uhalifu hususani madawa ya kulevya kuacha biashara hiyo ambayo inaharibu vijana wengi kwani wataendelea kuchukua hatua za kisheria dhidi yao.

Habari Zifananazo

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Oldest
Newest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Thelmairanda
Thelmairanda
17 days ago

I’ve gained only within four weeks by comfortably working part-time from home. Immediately when I had lost my last business, mtg I was very troubled and thankfully
following website___________ http://Www.Careers12.com

Last edited 17 days ago by Thelmairanda
Angila
Angila
17 days ago

Making every month extra dollars by doing an easy job Online. Last month i have earned and received $18539 from this home based job just by giving this only mine 2 hrs a day. Easy to do work even a child can get this and start making money Online. Get this today by follow instructions
.
.
.
On This Website……………..> > http://remarkableincome09.blogspot.com

Scholarship ya Mwanadamu mwenye
Scholarship ya Mwanadamu mwenye
16 days ago

Scholarship ya Mwanadamu mwenye akili ya ‘Kinyonga mdogo zaidi duniani’ aliyegundulika Tanzania

Kinyonga kwa jina Brookesia urefu wake ni milimita 13.5

Wanasayansi wanaamini kuwa wamebaini kinyonga mdogo zaidi duniani ambaye ukubwa wake ni sawa na mbegu.

Vinyonga hao wawili ilibainika nchini Madagasca na timu ya sayanasi ya Ujerumani na Madagasca.

Kinyonga wa kiume aliyepewa jina la Brookesia urefu wake ni milimita 13.5.
Na kinyonga huyo anakuwa mdogo zaidi kati ya spishi karibu 11,500 za vinyonga, kulingana na rekodi ya hifadhi ya wanyama ya taifa ya Bavaria katika mjini mkuu wa Munich.

Urefu wake kutoka juu hadi chini ni milimita 22.
Kinyonga wa kike ni mkubwa kidogo takribani milimita 29, taasisi hiyo imesema, ikiongeza kwamba aina nyingine bado hazijapatikana, licha ya kwamba “juhudi zimekuwa zikiendelea”.

“Kinyonga huyo mpya aliyepatikana kaskazini mwa Madagascar eneo la msitu linalopokea mvua kubwa, huenda yuko katika hatari ya kutoweka,” kulingana na jarida la wanasayansi.

Oliver Hawlitschek, mwanasayansi wa kituo historia huko Hamburg, alisema: “Kwa bahati mbaya eneo alilokuwa akiishi mjusi huyo lilianza kuingiliwa na binadamu lakini likaanza kulindwa hivi karibuni, kwahiyo anawezaa kunusurika.”

Watafiti walibaini kwamba kinyonga huyo alikuwa anatafuta mchwa katika msitu wenye mvua kubwa na kujificha dhidi ya wanyama wala nyama usiku kwenye nyasi.
Katika msitu ambao mjusi Brookesia alipatikana umepakana na misitu mingine kaskazini mwa kisiwa, walisema.

Katika ripoti yao, wanasayansi wamependekeza kuwa kinyonga huyo aorodheshwe kama mnyama aliye hatarini katika orodha ya Shirika la IUCN, linalochunguza hali ya maelfu ya jamii za wanyama kumsaidia kumlinda na makazi yake.

Back to top button
3
0
Would love your thoughts, please comment.x
()
x