Pasaka inawakumbusha kuishi kwa upendo

WAZIRI Mkuu, Dk Mwigulu Nchemba amesema kuwa pasaka ni kipindi muhimu kinachowakumbusha Watanzania kuishi kwa upendo, mshikamano na kudumisha amani katika jamii. Dk Mwigulu amesema hayo kwenye Tamasha la Pasaka la Mtoko na Christina Shusho lililofanyika Mlimani City Dar es Salaam.

“Amani si kwa ajili ya faida ya rais wala serikali, bali ni kwa ajili ya kila mwananchi. Pasipo amani hata shughuli ndogo kama kujitafutia kipato haziwezi kufanyika” SOMA: Dk Mwigulu: Amani ni msingi wa maendeleo

Ameeleza kuwa mnufaika wa kwanza wa amani ni mwananchi mwenyewe, kwani bila utulivu hata shughuli za kiuchumi, kijamii na ibada haziwezi kufanyika ipasavyo. Amempongeza mwimbaji wa muziki wa Injili, Christina Shusho kwa kuandaa tamasha hilo kubwa lililovuta maelfu ya waumini, akisema mafanikio yake yanaonesha kuwa lina kibali cha Mungu. “Ukiona jambo linafanikiwa kiasi hiki, ujue lina kibali cha Mungu. Serikali haitakuwa kikwazo katika mipango ya kuendeleza huduma ya injili,” alisema.

 

 

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

  2. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity……….
    .
    This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button