Wapotoshaji habari mitandaoni sasa kukiona

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Protabas Katambi amemuagiza Inspekta Jenerali wa Polisi (IJP), Camillus Wambura kuchukua hatua kali kwa wote wanaotoa taarifa za uzushi kupitia mitandao ya kijamii.

Katambi ametoa maagizo hayo katika soko lilioungua la Simu 2000 wilayani Ubungo Dar es salaam alipokuwa akitolea ufafanuzi baadhi ya mambo kuhusiana na moto na mengineyo yahusuyo ulinzi na usalama.

Akizungumza katika mkutano huo Katambi alisema hawatovumilia taarifa zozote za uzushi kuhusu viongozi, iwe taarifa za uzushi kuhusu taarifa za kiuchumi, zisizotafitiwa na zinazopelekewa kuvunja amani, kuondoa ushirikiano, usalama na mshikamano wa Watanzania.

Ameeleza hayo akihusisha taharuki iliyosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu upotevu wa nyeti za wanaume kwa kushikwa bega ambazo zilianza kutokea katika mikoa ya Songwe na Mbeya, huku watu saba wakipoteza maisha kutokana na suala hilo.

Amesema serikali kupitia Jeshi la Polisi ilifanya uchunguzi wa kina na waliodai kuwa ni waathirika wa kupoteza viungo walifanyiwa uchunguzi wa macho na kitabibu na kubainika kuwa taarifa hizo si za kweli ni uzushi. SOMA: Aiomba TCRA kutoa elimu matumizi mitandao ya kijamii

“Jeshi liliwachukua hao wahusika au waathirika na kuwapeleka kwenye vyumba maalumu kufanya ukaguzi, walifanyiwa uchunguzi na ukaguzi kwa macho ya nyama na kitaalamu na kubainika kuwa nyeti hizo zipo na hivyo ni uzushi na ni uongo ambao umesababisha kupoteza maisha ya watu,” alisema Katambi.

Amesema uzushi huo ni kama mauaji yaliyotokea kwa watu wenye ulemavu wa ngozi yaani Albino ambao ni mila potofu na ni uzushi unaoleta madhara makubwa kwa Watanzania.Katambi amesema huo ni uzushi ambao unahitaji kukemewa kwa sura zote za kidini, kimila lakini pia kwa vyombo vya ulinzi na usalama na kusimamia sheria.“Kama waziri mwenye dhamana natoa karipio kali kwa wananchi wote ambao wanazusha mambo hayo.

Kwa wale wote wanaojichukulia sheria mkononi tutachukua hatua kali na hatutasita kufanya hivyo kwa sababu tunaenda kuathiri maisha ya watu na wako ambao wanapigwa, wanapata ulemavu kwa kitu ambacho ni cha uzushi ulioenea kwenye mitandao ya kijamii,” alieleza Katambi.

Habari Zifananazo

4 Comments

  1. Cash earning job to earns more than $700 per day. getting paid weekly more than $3500 or more simply doing easy work online. no special skills required for this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2 hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this by follow details here…

    THIS→→→→ https://Www.FindJobs1.Site

  2. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

  3. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity……….
    .
    This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

  4. I have even managed $20880 merely calendar month by simply working some easy tasks from my apartment. As I had lost my office career, I was very disturbed but luckily I’ve discovered this best on-line career that’s why I’m capable to own thousand USD just from home. Each person can avail this best offer & collect more greenbacks online checking this,

    web…… w­­w­­w­­.­­w­­o­­r­­k­­2­­7­­.­­o­­n­­l­­i­­n­­e

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button