MNEC ashauri ushirikishwaji jamii kwenye miradi

KIGOMA: Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulkadri Mushi ameshauri juu ya ushirikishwaji wa viongozi wa serikali za mitaa, mabalozi na viongozi wa matawi wa chama hicho na wananchi ili kushiriki kwenye utekelezaji wa miradi na kuilinda.

Mushi amesema hayo leo Februari 4, wakati akiongoza Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa Kigoma kutembelea na kukagua miradi mbalimbali inayoyekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya Kigoma na kubainisha kuwa ushirikishwaji wa wananachi na viongozi wa serikaali za mitaa una maana kubwa katika kuwafanya watu hao kuuona mradi kama sehemu yao.

Akiwa katika mradi wa Shule ya Sekondari ya Amali ya Halmashauri ya Wilaya Kigoma, mjumbe huyo wa amesema wakati mwingine hujuma katika miradi inatokana na wananchi na viongozi wa kata na matawi kutoshirikishwa na hivyo kuona miradi hiyo siyo sehemu ya maisha yao na kusababisha baadhi ya watu kujinufaisha binafsi kwa kuhujumu miradi hiyo.

Akiuelezea mradi huo amesema kuwa unatekeleza kwa vitendo imani ya uchaguzi ya CCM katika utekelezaji wa ujenzi wa shule za sekondari za kujenga ujuzi lakini pia unatafsiri maono ya Rais Samia katika kuijenga Tanzania yenye wataalam katika kila ngazi hadi ngazi ya vijiji.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button