Uhifadhi wa Historia Kipaumbele Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali inaendelea kuweka mkazo katika uhifadhi na uimarishaji wa maeneo ya kihistoria kwa lengo la kulinda utamaduni na kukuza uchumi wa Zanzibar.
Akizungumza Ikulu Zanzibar Aprili 1, 2026, alipokutana na Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania, Marjo Crompvoets, Rais Mwinyi amesema juhudi hizo zinahusisha pia ukarabati wa Sinema ya Majestic unaofanyika kwa ushirikiano na Japan kwa lengo la kuhifadhi hadhi yake ya kihistoria na kuongeza matumizi ya kiutamaduni.

Ameishukuru Uholanzi kwa ushirikiano uliopo na kuwahimiza wawekezaji kutoka nchini humo kuja kuwekeza Zanzibar katika sekta za utalii, uchumi wa buluu, viwanda, uvuvi na kilimo. Kwa upande wake, Balozi Crompvoets ameahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano huo na kuongeza uwekezaji, akieleza kuridhishwa na kasi ya maendeleo ya kiuchumi Zanzibar. SOMA: Wawekezaji Ufaransa Waalikwa Zanzibar
Katika hatua nyingine, Rais Mwinyi amekutana na Balozi wa Slovakia nchini Tanzania, Ivan Lančarič, ambapo ameonesha utayari wa Zanzibar kushirikiana na nchi hiyo katika sekta za uwekezaji, biashara na utalii. Naye Balozi Lančarič amesema Slovakia inapanga kufungua ubalozi nchini Tanzania pamoja na ofisi ndogo Zanzibar ili kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na uwekezaji kati ya pande hizo.





My income reached $17,620 last month, thanks to a flexible online job. It’s astonishing how easy it is to get started and see real results. I spend my mornings working and still have the whole day to relax. The extra money has made a big difference in my financial situation. It’s a fantastic way to boost your income without overworking yourself..
Visit This…… www.work27.online