Iran, Israel zazidisha mashambulizi ya makombora

MAPIGANO kati ya Iran na Israel yameendelea huku pande hizo zikishambuliana kwa makombora na droni. Hatua hiyo inakuja wakati Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likitarajiwa kupiga kura kuhusu usalama wa mlango-bahari wa Hormuz.

Iran imesema bado ina uwezo mkubwa wa kijeshi licha ya kauli ya Donald Trump kuwa umeathirika. Israel imedai kumuua kamanda wa Iran, Jamshid Eshaghi, katika shambulio la Tehran. Nchini Lebanon, watu 27 wameripotiwa kuuawa katika mashambulizi dhidi ya makundi yanayoungwa mkono na Iran.

Pia, mashambulizi ya anga ndani ya Iran yamelenga miundombinu muhimu na kusababisha vifo na majeruhi. Iran imekosoa mashambulizi hayo ikisema hayatailazimisha kusalimu amri. Wakati huo huo, waasi wa Kihouthi nchini Yemen wamesema wamerusha makombora kuelekea Israel kwa kushirikiana na Iran na Hezbollah. SOMA: Iran yaikosoa Israel kuhusu usitishaji mapigano

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 12000-16700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern…………………… http://Www.Cash54.Com

  2. I just came across this amazing way to earn $11,000-$15,000 a month online! No selling, no struggle—just a simple system that anyone can follow. Mia Westbrook did it, and so can you! Don’t miss out on this life-changing opportunity.
    .
    This is what I do…………………… http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button