Bil 27/- kutekeleza miradi ya maendeleo Kahama

NAIBU Waziri  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  (Tamisemi) Zainabu Katimba amesema miradi  yote kwa Manispaa ya Kahama itatekelezwa kwa  jumla ya Sh bilioni 27.4

Waziri huyo leo Desemba 4 ameshuhudia hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa stend  ya mabasi  eneo la  Mbulu, Soko la Sango pamoja na ujenzi wa stend ya mabasi madogomadogo na soko la wajasiriamali eneo la Zongomela iliyofanyika katika eneo linalotarajiwa kujengwa Stendi Kuu Mbulu Kata ya Muhongolo.

Waziri Katimba amesema kutajengwa vizimba, migahawa na maeneo ya kupumzikia pamoja kituo cha polisi  hivyo hawana mashaka na mkandarasi aliyesaini mkataba na  utatekelezwa kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Desemba 2024 hadi Desemba 2025.

Mwakilishi wa Mtendaji  Mkuu  wa Tarura, Humprey Kanyenye akisoma taarifa ya namna ya utekelezaji  wa Miradi ya TACTIC amesema  miji 45 inatekeleza miradi hiyo  na imegawanywa katika makundi matatu lengo la  kuwepo mradi ni kuboresha miundombinu  mbalimbali na Kwa Kahama Mradi unatiwa saini leo ukikamilika utaongeza mapato kutoka Sh milioni 11 hadi kufikia Sh milioni 31.

Mbunge wa Jimbo la Kahama Mjini Jumanne Kishimba amesema leo wamekuja kushuhudia utiaji saini  Mkataba  kwani wanashida na barabara  mji unapanuka na watu wanaongezeka.

“Ngoja nisema waziri huyu mkandarasi mliyempa kujenga barabara tangu alivyosaini mkataba amekuwa wa kusuasua  alikuwa na greda moja kwenye eneo la kazi alivyoona unakuja ameongeza greda hivyo hatufai au serikali imsimamie kwa kumsukuma ili kazi iendelee,” amesema  Kishimba.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kahama, Thomas Muyonga amesema mradi huo ni wakanzwa  kutekelezwa kwa  Manispas ya Kahama hivyo aliomba watakao tekeleza wakandarasi watumie vibarua wazawa  na watumie uzalendo wa kutochelewesha mradi.

Habari Zifananazo

Back to top button