Kubecha akabidhiwa ofisi Gairo

MOROGORO: MKUU wa Wilaya Mteule Wilaya ya Gairo mkoani Morogoro, Japhari Kubecha amekabidhiwa rasmi ofisi na Mkuu wa Mkoa Mteule wa Songwe, Jabir Makame.

Makabithiano hayo yameshuhidiwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Gairo ,Kamati ya Usalama Wilaya , Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Gairo wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya na Kaimu Mkurugenzi na maafisa tarafa.

“Nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuniamini,” ameandika DC Kubecha.




