Madiwani Mikindani wamchagua meya mpya

MTWARA: HALMASHAURI ya Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara imefanya uchaguzi wa meya na naibu meya ambapo diwani wa kata Jangwani, Saidi Zaidi ameibuka mshindi katika nafasi ya umeya kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).
Hayo yamejiri leo Disemba 4, 2025 wakati wa mkutano wa kwanza wa Baraza la Madiwani la manispaa hiyo uliyofanyika kwenye manispaa hiyo.

Aidha, baraza hilo mbali na kufanyika kwa uchaguzi huo lakini limehusisha kiapo cha madiwani hao, uundaji wa kamati za kudumu za halmshauri, kupokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli za halmashauri zilizofanyika katika kipindi ambacho baraza la madiwani lilivunjwa na mengine.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Richard Mwalingo amesema idadi ya wapiga kura ilikuwa 24 hivyo amemtangaza Said Zaid kuwa mshindi wa kura zote zilizopigwa kutokana hakuna kura iliyoharibika wala hapana.
Nafasi nyingine ni naibu meya iliyogombewa na diwani wa kata Majengo, Sixmund Lungu aliyetetea kitu chake hicho kwa kipindi kingine tena aliyeibuka na ushindi wa kura zote kutokana na idadi ya wapiga kura hao kwani hakuna kura iliyoharibika wala hapana.

Akitoa shukrani kwa wapiga kura hao, meya huyo wa manispaa hiyo “Niwashukuru sana wajumbe kwa kuniamini na kunichagua kwa kura nyingi na naahidi kutekeleza majukumu haya kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopangwa kikubwa naomba ushirikano”
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mtwara Mjini, Salum Naida amesema wananchi wa mtwara mjini wamewachagua madiwani hao kutokana na kukiamini chama kwani hilo ni deni kubwa kwa wananchi hivyo wakawatumikie kikamilifu.




Mitandao ya kijamii ni fursa yakukuza uchumi wako. Kipaji chako ni bidhaa yako mtandaoni. Mawasiliano ni fursa.
I am making a good salary from home $7580-$9065/week , which is amazing, under a year ago I was jobless in a horrible economy. I thank God every day I was blessed with these instructions, Definitely a try..
See This Link………………………………….. http://Www.Cash43.Com
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com
Epuka kujiunga au kushiriki kwenye makundi ya mtandaoni yanayochochea vurugu. Ni kosa kwa mujibu wa sharia.