Mbio nishati safi zafana Arusha

ARUSHA: Mbio za Nishati Safi ya Kupikia zimemalizika jijini Arusha zikiwa na lengo la kuhamasisha, kutoa elimu  na mafunzo juu ya matumizi ya nishati salama.

Mbio hizo zimehusisha washiriki 350  kutoka  maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya Arusha washindi  watano katika mbio za km 21,km10 na km 5 walikabidhiwa zawadi za majiko ya gesi pamoja na umeme.

Mwandaaji wa mbio hizo Noureen Mawalla kutoka Tabwa  amesema Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia itaendeshwa katika kanda tano na sasa imemalizika kanda ya.Kaskazini  kwa watu 350 kushiriki na sasa itafanyika Kanda ya Ziwa na kanda ya kati.

“Mwitikio ni mkubwa watu wanaweza kujifunza na kupata uelewa kwani awali walikuwa hawaelewi ila sas tunaona mwamko mkubwa katika matumizi ya nishati safi na hii ni kutokana na elimu inayoendelea kutolewa,”alisema Mawalla.

Ameongeza kuwa  matarajio yao ni kuendelea kuhamasisha kupitia michezo kwa maana ya  mbio na aliwashukuru wote waliohusika kufanikisha .

Akizungumza katika mbio hizo  Mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Nishati safi ya kupikia kutoka Wizara ya nishati  Nolasco  Mlay amesema wao kama serikali wanaendelea kutoa mkato na msisito katika matumizi sahihi ya Nishati hii salama.

Alisema kwa mujibu wa takwimu watu 33,000 kila mwaka  wanakufa kutokana na nishati isiyo salama hivyo ni wajibu wetu kuendelea kutumia nishati safi kwa kutoa elimu kote.

“Rais wetu ndio kinara wa kampeni hii ya matumizi ya Nishati safi kwani itatusaidia kuhakikisha tunalinda afya na  mazingira yetu na  kama Wizara malengo  yetu ifikapo mwaka 2034 asilimia 80 tuwe tanatumia nishati safi,”alisema Mlay.

Naye Ofisa Michezo wa jiji la Arusha Benson Maneno amesema kama serikali inatoa shukrani kwa waandaaji  kutokana na kutumia vitu vya maendeleo katika kuelimisha jamii juu ya umuhimu wa nishati safi.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button