ICRC yakosoa mpango wa Israel

GAZA, PALESTINA: KAMATI ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) imesema mpango wa Israel wa kupanua mashambulizi Gaza ni hali isiyovumilika.
Msemaji wa ICRC, Christian Cardon, amesema kuongezeka kwa mapigano kutawaacha maelfu bila makazi, kuongezeka kwa maafa ya kibinadamu ambalo tayari limeathiri mamilioni. SOMA: Israel yaendeleza mashambulizi
Israel imetangaza kuwaita askari wa akiba 60,000 kushiriki katika operesheni hiyo huku ICRC ikiendelea kusisitiza umuhimu wa kulinda raia na kuendelea kuratibu ubadilishanaji wa mateka.



