Wakulima wadogo wafaidika na kilimo Ekolojia

MTANDAO wa wakulima Afrika Mashariki na Kusini (ESAFF) umesema umefanikiwa kuwafikia wakulima wadogo zaidi ya milioni tatu nchini Tanzania kupitia kilimo ekolojia, kwa kuwaunganisha kushiriki vikao vya kuibua vipaumbele, vikao vya bajeti na mafunzo ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Hayo yalibainishwa jijini Nairobi na Meneja wa Programu wa ESAFF, Emanuel Justine, wakati wa warsha iliyokutanisha wakulima wadogo, wadau wa kilimo na waandishi wa habari kutoka ukanda wa Afrika Mashariki.
Alisema ESAFF inashirikiana na Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) kuhakikisha wakulima hao wanapata fursa za mafunzo, uragibishi wa sera na kushiriki katika maamuzi ya kisera yanayohusu sekta ya kilimo. SOMA: Viongozi mitaa watakiwa kutoa elimu ya mazingira
“Lengo la warsha hii ni kujifunza pamoja, kutathmini changamoto za wakulima wadogo na kuangalia namna tunaweza kushirikiana na vyombo vya habari kusukuma ajenda ya mabadiliko ya tabianchi kuanzia ngazi ya kijiji hadi kimataifa,” alisema Justine.
Uwekezaji katika kilimo ekolojia
Justine alisema kilimo ekolojia kikiwekewa uwekezaji wa kutosha kinaweza kuwa suluhisho endelevu dhidi ya changamoto za mabadiliko ya tabianchi. Alieleza kuwa wakulima wadogo wengi wameshaanza kutumia mbinu hizo ikiwamo kuchanganya mazao, kutengeneza mbolea kutokana na samadi na taka za nyumbani.
“Ni muhimu mamlaka kutambua ukweli wa changamoto zinazowakabili wakulima wadogo na kufanya marekebisho ya sera yanayowaunga mkono. Hii ndiyo njia ya kuhakikisha wakulima wanaendeleza uzalishaji wa chakula,” alisisitiza.
Alibainisha kuwa wakulima wadogo huzalisha asilimia 80 ya chakula duniani, huku vyakula vya kilimo ekolojia vikiwa na uhitaji mkubwa katika masoko ya kimataifa. Hata hivyo, bidhaa zinazotumia viuatilifu na mbolea za kemikali hukataliwa katika baadhi ya nchi zilizoendelea.
Ushiriki wa kijamii na kiuchumi
Mbali na kushiriki katika vikao vya bajeti na kupanga vipaumbele, alisema wakulima wadogo kupitia MVIWATA wameanzisha vikundi vya akiba na mikopo (SACCOS), vinavyowawezesha kupata mitaji na kufanya biashara kwa pamoja.
Kwa upande wake, Rais wa Shirikisho la Wakulima Afrika Mashariki (EAFF) kutoka Uganda, Elizabeth Msemadala, alisema mabadiliko ya tabianchi yameendelea kuwa changamoto kubwa kwa wakulima barani Afrika kutokana na kilimo kutegemea zaidi mvua.
“Zaidi ya asilimia 80 ya kilimo chetu kinategemea mvua, lakini rasilimali za kusaidia wakulima hazifiki ipasavyo. Ndiyo maana tumeungana katika kampeni hii ya hatua za hali ya hewa kwa wakulima wadogo ili kuwa na sauti moja kimataifa,” alisema.
Msemadala aliongeza kuwa changamoto zinazowakabili wakulima Afrika zinatofautiana na zile za mabara mengine, hivyo ni muhimu kuweka mikakati mahsusi ya kikanda ili kuhakikisha sekta ya kilimo inakua na kuchangia maendeleo ya kiuchumi.
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→→→→→→→ http://Www.Payathome9.Com
JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
.
This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com