Kiruswa aishukuru serikali ya CCM kuthamini wafugaji

ARUSHA : MGOMBEA ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Longido, Dk Steven Kiruswa ameishukuru serikali kwa kuithamini sekta ya mifugo na wafugaji. Dk Kiruswa alisema hayo katika Uwanja cha Sheikh Amri Abeid Arusha kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Samia Suluhu Hassan.
Amesema Rais Samia akiwa madarakani, ndiye kiongozi aliyetambua umuhimu ya wananchi wa jimbo hilo ambao asilimia kubwa ni wafugaji, kwa kumtuma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa kutangaza kwamba maeneo yao ya malisho yatabaki kuwa salama.
“Wafugaji ambao ndio asilimia kubwa ya jamii ya jimbo hili wanakuomba watakapokuchagua tena, wanaomba maeneo yao yapimwe, yasajiliwe na wasaidiwe miradi ya maji kwa ajili ya mifugo yao kama mabwawa na visima virefu na kuendelea kuwatengea maeneo ya ufugaji,” alisema Dk Kiruswa.
Alisema serikali ya Rais Samia imefanya maboresho mengi kwenye sekta ya nishati, ambayo umeme umefika kila kijiji na hata katika maeneo yenye migodi. Dk Kiruswa alisema katika miaka minne ya uongozi wake, alitoa Sh bilioni 26 kwa ajili ya kujenga mradi wa maji kutoka Mlima Kilimanjaro kwenye Mto Simba kwenda Longido hadi Namanga na tayari aliuongezea thamani mradi huo kwa kutoa Sh bilioni 14 zilizoelekezwa kwenye chanzo cha maji Bonde la Sinya. SOMA: Kinana amsifu kwa bidii Samia
“Longido ambayo ilikuwa ni moja ya wilaya zenye ukame nchini, ulipoingia madarakani upatikanaji wa maji katika maeneo ya vijiji na miji ulikuwa ni asilimia chini ya asilimia 56 lakini sasa umefikia zaidi ya asilimia 70,” alisema. Pia, alisema wananchi wa Longido wameamua na wamedhamirimia kumchagua kwa asilimia 100, kwa sababu jimbo hilo lilishaweka historia ya kukipigia kura chama hicho kwa asilimia zote.
Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
.
More Details For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com
Cash earning job to earns more than $300 per day. getting paid weekly more than $2300 or more simply doing easy work online. no special skills required for this job and regular earning from this are just awesome. all you need is 2 hrs a day for this job and earning are awesome. every person can get this by follow details here…
.
.
HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com