‘Kairuki ni lulu msiipoteze Kibamba’

DAR ES SALAAM; MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT), Hawa Ghasia amesema mgombea wa Jimbo la Kibamba kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Angellah Kairuki ni lulu ambayo wanakibamba hawapaswi kuipoteza kutokana na uwezo wake mkubwa wa kusimamia,kufuatilia na kutekeleza miradi ya maendeleo.

Amesema Kairuki ana uwezo wa kuieleza vizuri Ilani ya CCM,  hivyo haendi kujifundisha ubunge anaujua amekuwa mbuge mara kadhaa hivyo wakimchagua hana pa kwenda kuuliza anajua na pia ni mfuatiliaji.

Amesema haya wakati akimnadi mgombea huyo katika mkutano wa kampeni za jimbo hilo zilizofanyika katika kata ya Goba jijini Dar es Salaam na kusisitiza kuwa Oktoba 29 wananchi hao wakapige kura kuichagua CCM.

“Amekuwa waziri kwa miaka mingi , amekuwa mjumbe wa haki za binadamu akiiwasilisha Afrika kwenye bunge la dunia na ni mshauri wa Rais ana sifa nyingi Angellah amepewa kila kitu ana akili njema na kapewa kila kitu. Wanakibamba msiipoteze lulu mliyopata,” amesema na kuongeza:

“Ninamuombea kura mgombea urais  Dk Samia Suluhu Hassan, Mbunge na diwani wote wa chama cha Mapinduzi tunaomba kura kwa mafiga matatu kazi aliyofanya Samia kwa miaka minne imefanya Chama Cha Mapinduzi kimpitishe kama mgombea pekee, amepeleka shule kila kijiji, hospitali za kutosha, zahanati na maji ya kutosha.”

Kwa upande wake mgombea udiwani wa kata ya Goba, Laurence Mlaki ameomba wananchi wa kata hiyo kumchagua ili aweze kushirikiana na mbunge kutatua kero zilizopo.

Habari Zifananazo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button