Mwinyi kufanya mageuzi ya kilimo

MGOMBEA wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameahidi kuinua uchumi wa wakulima na wavuvi kupitia mageuzi makubwa katika sekta za mwani, mpunga na uvuvi, ikiwemo kuongeza bei ya mwani kutoka shilingi 700 hadi 1,000 kwa kilo.

Akizungumza na wakulima wa mpunga wa Cheju, wakulima wa mwani na wavuvi katika uwanja wa Marumbi, Mkoa wa Kusini Unguja, Dk. Mwinyi alisema serikali tayari imetenga fedha kwa ajili ya kununua mwani wote uliopo majumbani kwa bei mpya, akisisitiza kuwa sekta hiyo ni nguzo muhimu ya uchumi wa buluu.

Alisema Zanzibar inaongoza barani Afrika kwa uzalishaji wa mwani, hivyo serikali itaendelea kuboresha miundombinu, masoko na teknolojia za kisasa ili kuongeza tija na kuwasaidia wakulima kunufaika zaidi na zao hilo. “Tutahakikisha tunanunua mwani wote na kujenga viwanda vya kuusindika kama tulivyofanya Pemba, ili kuongeza thamani na kipato kwa wakulima,” alisema.

Akizungumzia kilimo cha mpunga, Dk. Mwinyi aliahidi kuendelea kuboresha miundombinu ya mabonde yote ya mpunga, pamoja na kuongeza idadi ya matrekta, mashine za uvunaji na pembejeo bora ili wakulima wazalishe kwa wingi na kutumia teknolojia ya kisasa. SOMA: Tabianchi Yatikisa Kilimo cha Mwani

Alisema Zanzibar bado inaagiza mchele kutoka Tanzania Bara na nje ya nchi, hivyo kuna haja ya kuhakikisha uzalishaji wa ndani unaongezeka kwa ajili ya usalama wa chakula. Aidha, Dk. Mwinyi aliahidi kuendelea kutoa mikopo isiyo na riba kwa wakulima na wavuvi na kuondoa urasimu katika upatikanaji wake, akisisitiza kuwa sekta hizo tatu ni msingi wa uchumi wa buluu.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk. Mohammed Said Dimwa, alisema Dk. Mwinyi ni kiongozi mwenye maono ambaye ameleta mabadiliko makubwa ya maendeleo na kuwataka wananchi kumpa ridhaa tena katika uchaguzi wa Oktoba 29.

Wakulima na wavuvi walimpongeza Dk. Mwinyi kwa hatua za kuimarisha sekta zao, huku Fatma Abdalla, mkulima wa mwani, akiomba serikali kuendelea kuwapatia vifaa vya kilimo cha mwani na kuongeza bei ya zao hilo, na Ali Nassor wa Chwaka akitaka serikali ijikite zaidi kwenye uvuvi wa bahari kuu na udhibiti wa uvuvi haramu.

Habari Zifananazo

3 Comments

  1. JOIN US Everybody can earn 250/h Dollar + daily 1K… You can earn from 6000-12700 Dollar a month or even more if you work as a part time job…It’s easy, just follow instructions on this page, read it carefully from start to finish… It’s a flexible job but a good earning opportunity. tab for more detail thank you……..
    .
    This is my main concern……………………………………. http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

  3. I­ g­­­­­e­t­­­­ p­a­i­­­d­­­­­­­ o­­­­­v­e­r­ 2­­­2­­­0­­­ D­­­o­­­­­­lla­­­r­­­­­s p­­­­­e­­­­­r­ ­­­h­o­­­­­u­r­­­ ­­­­w­­­­o­r­k­­i­­­­n­g­ f­r­o­­m­ h­o­m­e­ ­w­i­t­h­­ 2 k­i­d­­s­ a­t­ h­o­­m­e­. i­ n­e­v­e­r­ t­h­o­u­g­h­t­ i­’d­ b­e­ a­b­l­e­ t­o­ d­o­ i­t­ b­u­t­ m­y­ b­e­s­t­ f­r­i­e­­n­d­ e­a­r­­n­s­ o­v­­e­r­ 1­5k­ a­ m­­o­n­t­h­ d­­o­i­n­g­ t­h­­i­s­ a­n­d­ s­­h­e­ c­o­n­v­i­n­c­­e­d­ m­e­ t­o­ t­r­­y­. it was all true and has totally ch­a­n­g­e­d­ ­m­y­ l­i­f­e­. T­h­i­s­­ ­i­s­ ­w­h­a­t­­ ­I­ ­d­­o­­­­­­­,­­­­­­­ ­c­h­­­­­e­­­­c­­­­k­ ­­­­i­­­­t­ ­o­­­­­u­t­ ­­­­b­y­ ­­­­V­i­s­­­­­i­t­i­n­­­­g ­F­o­­­­l­l­o­w­i­­n­­­­­g ­W­e­b­s­­­­­i­t­e

    ­
    Open This…. https://Www.Work99.site

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button