Wagombea CCM waahidi kliniki za kibingwa

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Geita mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhandisi Chacha Wambura amesema akichaguliwa anatamani kuona kliniki za madaktari bingwa zinafika vituo vya afya.

Mhandisi Chacha amesema hayo wakati akinadi sera na kuomba kura za chama hicho katika kata ya Nyanguku iliyopo Manispaa ya Geita kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 29, 2025. Amesema iwapo atapewa rdihaa ya kuwa mbunge wa jimbo la Geita mjini atashawishi uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kupanga utaratibu wa madaktari bingwa kufanya kliniki kwenye vituo vya afya.

Amesema hatua hiyo itasaidia kupunguza adha ya wananchi kutumia gharama kubwa kufuata vipimo na matibabu ingali tayari serikali inatumia gharama kubwa kujenga miundombinu ya vituo vya afya. Amesema ilani ya CCM 2025-2030 inaonyesha tayari serikali imeshatenga kiasi cha sh milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Nyankungu ili kusogeza huduma bora za afya.

Aidha Mhandisi Wambura amesema bado pia kuna kazi kubwa ya kufanya kuhakikisha Manispaa ya Geita inakuwa kinara kwenye sekta ya elimu kwa kuhakikisha ubora wa elimu unaendana na majengo yaliyopo. “Tuna mpango wa kuhakikisha Geita (Manispaa) inaongoza kwa suala la elimu, tunataka tuongoze hapa Geita (mkoa) harafu wengine wafuate”, amesema Mhandisi Wambura.

Mgombea Udiwani wa CCM kata ya Nyanguku, Elias Ngole amekiri kuwa kwa sasa kazi kubwa imefanyika kujenga majengo ya kisasa kwenye zahanati na vituo vya afya lakini kuna uhitaji mkubwa wa matabibu. “Sipendi tujenge kituo cha afya kwa maana ya majengo, naomba tukajenge kituo cha afya kwa maana ya huduma, tukalete madaktari bingwa”, amesema Ngole. SOMA: Mwinyi: Hakuna atakayebaguliwa, wote ni wazanzibari

 

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
    .
    HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button