Wafanyabiashara wahimizwa kutumia bandari Tanzania

ZAMBIA: Balozi wa Tanzania nchini Zambia, Luteni Jenerali Mathew Mkingule, amewahimiza wadau na watumiaji wa bandari kuendelea kutumia bandari za Tanzania kama lango kuu la biashara kwa nchi za Ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika.

Akizungumza jijini Lusaka jana Oktoba 15, 2025 wakati wa ufunguzi wa Jukwaa la Wadau na Watumiaji wa Bandari za Tanzania, Balozi Mkingule amesema Tanzania ipo tayari kutoa huduma bora, za kisasa na zenye ushindani mkubwa kupitia Bandari ya Dar es Salaam na bandari nyingine za nchi hiyo.

Takwimu zinaonesha ongezeko la shehena ya mizigo kutoka na kuingia Zambia kupitia bandari za Tanzania kwa zaidi ya asilimia 55, kutoka tani milioni 2.2 mwaka 2023/24 hadi tani milioni 3.5 mwaka 2024/25, hali inayoashiria ufanisi mkubwa wa huduma zinazotolewa.

Ziara hiyo ya kimasoko nchini Zambia ni sehemu ya juhudi za Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa kushirikiana na DP World Dar es Salaam na TEAGTL katika kuimarisha uhusiano wa kibiashara wa kikanda na kuendeleza diplomasia ya kiuchumi.

Habari Zifananazo

2 Comments

  1. I get paid over (90$ to 500$ / hour ) working from home with 2 kids at home. I never thought I would be able to do it but my best friend earns over $22000 a month doing this and she convinced me to try. it was all true and has totally changed my life… This is what I do, check it out by Visiting Following web….
    .
    HERE——————————————⊃⫸ http://Www.Cash43.Com

  2. Google is now paying $300 to $500 per hour for doing work online work from home. Last paycheck of me said that $20537 from this easy and simple job. Its amazing and earns are awesome. No boss, full time freedom and earnings are in front of you. This job is just awesome. Every person can makes income online with google easily……….
    .
    M­­­­­­o­­­­­­r­­­­­­e­ D­­­­­­e­­­­­­t­­­­­­a­­­­­­i­­­­­­l­­­­­­s For Us→→→→ http://Www.Payathome9.Com

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Back to top button